Mawaziri kujadili upatikanaji taulo za kike


WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa amewataka wanasiasa waache kuingilia serikali inapotoa maagizo yenye tija kwa wananchi, likiwemo la kuwahamisha wananchi wa mabondeni.
Majaliwa amesema, wanasiasa wanapaswa kuiunga mkono Serikali kudhibiti maafa makubwa mvua zinaponyesha kwa wingi.
Ameeleza mikakati ya serikali kukabiliana na athari zilizotokana na mvua zinazoendelea kunyesha ikiwemo kuagiza kamati za maafa za mikoa kufanya tathmini ya athari hizo na mkakati wa serikali wa kujenga bonde la Msimbazi ambalo ni chanzo cha maafa jijini Dar es Salaam.
Ameyasema hayo leo bungeni mjini Dodoma wakati anajibu maswali ya papo kwa papo kutoka kwa wabunge. Wabunge walitaka serikali iainishe mikakati ya kukabiliana na athari hasa za miundombinu zinazosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha nchini.
Mbunge wa Nyang’wale Hussein Nassoro (CCM), wakati anauliza, alieleza namna mvua zilivyoleta maafa na kubainisha kuwa takribani asilimia 75 ya miundombinu nchi nzima imeathirika, huku wananchi wakipoteza mali zao na wengine kupoteza maisha.
“Tumepata bahati kutoka Mungu kwa mvua nyingi zinazoendelea kunyesha lakini pamoja na hali zimekuja na maafa makubwa, je serikali imepangaje kurejesha miundombinu hii katika hali yake ili wananchi waendelee na shughuli za maendeleo kama kawaida?” ameuliza Mbunge huyo.
Mbunge wa Temeke Abdallah Mtolea (CUF), alimuuliza Waziri Mkuu mikakati ya serikali kuhakikisha jiji la Dar es Salaam, halipatwi na maafa ya watu kupoteza maisha na miundombinu kuharibika kila mvua zinaponyesha.

Mawaziri kujadili upatikanaji taulo za kike Mawaziri kujadili upatikanaji taulo za kike Reviewed by KUSAGANEWS on April 19, 2018 Rating: 5

No comments: