Msanii Roma Mkatoliki
ametimiza masharti aliyopewa na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
Dkt. Harrison Mwakyembe kumtaka ajisajili Baraza la Sanaa la Taifa (BASATA) na
kuwa akifanya hivyo atakuwa ametambulika na kuwa huru kufanya kazi.
Roma Mkatoliki leo April 5, 2018
amekwenda Baraza la Sanaa la Taifa na kujisajili kama ambavyo aliagizwa na
viongozi wa serikali na kusema kuanzia leo atakuwa huru kufanya kazi na sasa
anarudi rasmi katika muziki.
Mar 1, 2018 Msanii wa muziki wa Hip
Hop bongo Roma Mkatoliki alifungiwa kufanya shughuli za muziki kwa muda wa
miezi sita kwa kile kilichodaiwa msanii huyo kudharua wito wa BASATA na Naibu
Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo.
Msanii huyo ametumikia kifungo hicho
kwa mwezi mmoja na siku tano hivyo kifungo chake kimeisha leo baada ya
kujisajili BASATA.
Msanii Roma Mkatoliki ajisajili na
kukabidhiwa rasmi cheti cha kutambulika na Baraza la sanaa la Taifa leo April
05 2018, Hii ni baada ya kupewa sharti na Wizara ya Habari ya kujisajili kwanza
Basata ili aondolewe adhabu yake ya kufungiwa miezi 6.
Roma aimiza masharti ya Serikali.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment