Mtu
mmoja aliyefahamika kwa jina la Mateso Milu Bujingi (35) ameuwawa na kundi la
watu waliojichukulia sheria mkononi kwa kumpiga mawe na fimbo sehemu mbali
mbali za mwili wake kwa kosa la kutapeli mbuzi wawili wenye thamani ya shilingi
elfu 55
Hayo
yamebainishwa leo na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Naibu Kamishna wa Polisi
Ahmed Msangi na kusema mbali na mtu huyo kuuwawa, Polisi walifanikiwa kumuokoa
Malecha Gilala (38) ambaye naye alikuwa anashirikiliana na marehemu kufanya
utapeli huo nyumbani kwa bwana Lubeja Tulu, kwa kujifanya wao ni maofisa wa
Polisi kuwa wamekwenda kwake kwa lengo la kumkamata kutokana na mgogoro wa
shamba uliopo kati yake na jirani yake na kutaka wapatiwe kiasi cha fedha laki
mbili ili wasiweze kumpeleka Polisi.
Aidha, Kamanda
Msangi amesema tukio hilo limetokea jana (Aprili 04, 2018) majira ya saa 11:30
jioni katika kijiji cha Nyanzumula kata ya Kagunga tarafa ya Nyanchenche wilaya
ya Sengerema mkoani Mwanza.
Inadaiwa kuwa
kutokana na Lubeja kutokuwa na fedha hizo aliwapa mbuzi wawili vijana hao ili
wasiweze kumkamata lakini kwa bahati mbaya matapeli hao walirudi siku nyingine
wakitaka wapatiwe tena ndipo Lubeja alipoamua kuenda kutoa taarifa kwa mwenyekiti
wa mtaa pamoja na Polisi lakini wakati askari walipokuwa wanafanya ufuatiliaji
wa kwenda eneo la tukio ghafla wananchi wenye hasira kali waliwavamia na kuanza
kuwashambulia matapeli hao na kupelekea mmoja kufariki wakati alipokuwa
akikimbizwa hospitalini kutokana na kipigo alichokipata.
Kamanda Msangi
amesema mpaka sasa hakuna mtu yeyote aliyefanikiwa kukamatwa kuhusiana na tukio
hilo, huku akitoa onyo kwa wananchi kuacha tabia ya kutumia majina ya vyombo
vya ulinzi na usalama katika kufanya uhalifu.
Auwawa kwa kosa la kutapeli Mbuzi ya shilingi 55 elfu
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment