Waziri wa Mambo ya Ndani
ya Nchi, Mwigulu Nchemba ameliagiza Jeshi la Polisi kuwatoza faini, kuwaweka
ndani madereva na wasiachiwe mpaka pale watakapo wafikisha Mahakamani pindi
watakapo wabaini wanaendesha vyombo vya moto kwa mwendokasi.
Mwigulu ametoa
kauli hiyo leo (Aprili 05, 2018) katika Mkutano wa 11 wa kikao cha Bunge cha
tatu kilichofanyika katika mkoa wa Dodoma wakati akitoa taarifa ya ajali
iliyotokea wilayani igunga jana kwa kuhusisha lori aina ya fuso na basi la
abiria la kampuni ya city boys na kuua watu 12.
"Taarifa
za awali tulizopewa kwamba chanzo cha ya ajali hiyo sio mashimo ya barabarani
pekee yake bali ni mwendo kasi wa dereva wa fuso ambaye alisababisha kuligonga
basi hilo hivyo naliagiza jeshi la polisi popote pale watakapomkamata dereva
anatembea mwendokasi pamoja na hiyo ya kutoza faini, wamuweke ndani wasimuachie
mpaka pale watakapompeleka Mahakamani ili hatua zaidi ziweze kuchukuliwa", amesema Mwigulu.
Pamoja na
hayo, Mwigulu ameendelea kwa kusema "endapo dereva huyo akitoka
Mahakamani na kama rekodi zake ni mwendokasi basi anyang'anywe leseni yake ili
asiweze kuendelea kuendesha magari yanayosababisha ajali na kupoteza maisha ya
watu kama hivi jana ilivyotokea".
Kwa upande
mwingine, Rais Magufuli amewataka viongozi wote wanaohusika na usimamizi wa usalama
wa barabarani kutafakari kwa nini ajali nyingi zimekuwa zikitokea katika maeneo
yaleyale na kutafuta ufumbuzi ili kuepusha madhara ya watu kupoteza maisha,
kupata ulemavu wa kudumu na kupoteza mali.
Mwigulu ataka Madereva kuwekwa ndani na wasiachiliwe
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment