Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Mrisho Gambo
amemwambia Rais John Magufuli kuwa atakuwa naye hadi atakapokufa, akimsaidia
katika vita ya kiuchumi
Gambo ameyasema hayo leo Aprili 7 katika
uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini Arusha wakati Rais Magufuli alipokuwa
akizungumza na wananchi baada ya kuzindua kituo cha polisi na nyumba 31 za
polisi
“Nikuhakikishie kuwa nitakuwa mtu wa mwisho
kufa hadi vita uliyoanzisha inafikia mwisho,”amesema.
Gambo amesema kuna watu ambao wanakwamisha
kwa makusudi juhudi za Rais na wanataka viongozi wengine wasimpe ushirikiano na
hivyo akasema yeye atakuwa pamoja na Rais Magufuli mpaka mwisho
“Nia yao ni kuona tunakuacha peke yako,
lakini hatutafanya hivyo, tutakuwa na wewe katika vita hii mpaka mwisho,”
amesema
Pia, amesema wapinzani wamekuwa
wakilalamikia mambo mengi ikiwamo suala la ndege, lakini ndege imekuja na bado
wanasema
“Umeleta ndege sita, sasa wanalalamika mbona
umenunua hii na kuacha kile. Hawa ni popo siyo ndege wala wanyama hivyo
usihangaike nao,” amesema na kuongeza
“Wapinzani wangependa wote tukate tamaa ili
ubaki peke yako, mimi kama msaidizi wako nakuhakikishia nitakuwa wa mwisho kufa
katika vita hii.”
Rc Gambo: Nitakuwa wa mwisho kufa katika vita vya uchumi
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 07, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment