Rais John Magufuli leo ametoboa siri kuwa
mke wake, Janeth alikuwa ni mtoto wa polisi
Ameyasema hayo leo Aprili 7 wakati wa
uzinduzi wa nyumba 31 za polisi mjini Arusha na kusema baba mkwe wake
alikuwa sajenti wa polisi
“Nyumba za polisi ndizo zimenipa mke kwa
hiyo nyumba za polisi ninazifahamu, huyu mke wangu niliye naye alikuwa mtoto wa
polisi, marehemu baba yake hakuwa na cheo kikubwa alifariki akiwa sajenti,”
amesema
Ameongeza kuwa, “Ingekuwa nazindua Moshi,
angenionyesha nyumba walizokaa lakini za Oysterbay alizoishi alishanionyesha na
za Ukonga na za sehemu nyingine. Kwa hiyo maisha ya polisi ninayafahamu.”
Amemtaka Mkuu wa Jeshi la Polisi (IGP),
Simon Sirro kuhakikisha polisi hao wanaingia kwenye nyumba zao kesho.
Raisi Magufuli atoboa Siri ya Yeye na Mkewe
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 07, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment