Siku chache baada ya Mwenyekiti wa Mtandao
wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo kuhojiwa na Idara ya Uhamiaji Mkoa wa
Dar es Salaam kuhusu uraia wake, baba yake Omar Nondo amefunguka kuhusu uraia
wa mtoto wake
Nondo ambaye pia ni mwanafunzi wa mwaka wa
tatu katika Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), amejikuta kwenye misukosuko na
vyombo vya dola tangu alipotoweka katika kile kilichoelezwa kuwa ni katika
mazingira ya kutatanisha Machi 6 na kuonekana Machi 7 wilayani Mufindi, Iringa
Baada ya Nondo kuripoti polisi mjini Mafinga
alishikiliwa na jeshi hilo Mkoa wa Iringa na na baadaye kukabidhiwa kwa Polisi
Kanda
Maalumu ya Dar es Salaam ambako kamanda wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa
alisema kupitia uchunguzi wa kisayansi, wamebaini kuwa hakuwa ametekwa, bali
alijiteka na tayari suala lake lipo mahakamani, Iringa
Jana mzazi wa mwanafunzi huyo alijitokeza
kuzungumzia suala la uraia wa mtoto wake na kueleza kwamba, baba yake (yaani
babu wa Nondo) alizaliwa mwaka 1919 huko Ujiji, Kigoma na kuwa ni miongoni mwa
waasisi wa chama cha Tanu
Mzee Omar, alisema baba yake huyo aliyemtaja
kwa jina la Omar Kagobe alipata watoto 30, mmoja akiwa yeye
“Nashangaa hao wanaomkamata na kumhoji mtoto
wangu kuwa sio raia, wananichekesha sana kwa kuwa najua mwisho wa siku watajua
ukweli wake
‘Ukweli ni kwamba wazazi wangu ndio waasisi
wa Tanu na walishiriki kikamilifu katika kupigania uhuru wa nchi hii, hivyo
suala hilo halinipi wasiwasi wala hofu na hivyo vyeti wanavyovitaka mbona vipo
tu, ila waelewe kuwa sisi ni Wamanyema halisi na ni raia halali wa nchi hii,”
alisema
Pia alisema babu yake Nondo, alishawahi kuwa
Polisi kwa miaka 18 kuanzia mwaka 1940 hadi 1958 na alishafanya kazi huko
Mabatini mkoani Mwanza na sehemu nyingine za nchi
Alisema babu yake Nondo akiwa polisi, ndipo
zilipoanzishwa Kota za Msimbazi, Dar es Salaam na jina lake lilikuwa maarufu,
akijulikana kama Mzee Kagobe
Kama haitoshi alisema bibi yake Nondo
alikwenda kuhiji, mnamo 1970 na alipewa hati ya kusafiria ya Tanzania, huku
akihoji, “Kama angekuwa sio raia wa Tanzania angepewaje hati hiyo?”
Hata hivyo, alibainisha kuwa anachopitia
mtoto wake kwa sasa ikiwamo kuitwa na Idara ya Uhamiaji, ni jambo
linalotengezwa na mtu binafsi
Juzi, Mwenyekiti wa ACT - Wazalendo, Mkoa wa
Kigoma, Sendwe Mbaruku, alitoa taarifa kuhusu suala la Nondo kuhojiwa na
uhamiaji na kusema; “Kijana Abdul ni mtoto wetu hapa Kigoma, wazazi wake ni
wakazi na wapiga kura wa hapa Ujiji, zaidi ni Watanzania wenzetu.”
Hivi karibuni Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto
Kabwe alituma taarifa kwenye mitandao ya kijamii akisema kwamba atawashtaki kwa
wazee wa Ujiji wale wote wanaohoji uraia wa kijana huyo.
Taarifa za kuhojiwa kwa Nondo zilitolewa
Machi 4 na Mtandao wa Watetezi wa Haki za Binadamu Tanzania (THRDC), kupitia
ofisa wake wa utetezi na ushwishi, Leopald Mosha
Mosha alisema kwamba Nondo aliitwa katika
ofisi ya Uhamiaji Mkoa wa Dar es Salaam zilizopo kwenye ofisi ya Wizara ya
Mambo ya Ndani na kuhojiwa kwa saa mbili kuhusu taarifa zake za uraia
Pamoja na kuwasilisha taarifa za wazazi
wake, alisema kijana huyo ametakiwa pia kuwasilisha vyeti vya kuzaliwa vya babu
na bibi yake wa pande zote mbili ifikapo Aprili 20 mwaka huu.
Baba yake Nondo afunguka sakata la uraia wa mwanaye
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 07, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment