Raisi Magufuli abadili maamuzi


Rais Dkt. John Magufuli amebadili maamuzi aliyotoa hivi karibuni ya kurejeshwa serikalini fedha zilizokuwa zimetolewa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Bumbuli iliyopo wilayani Lushoto mkoani Tanga na kutaka fedha hizo ziendelee kufanya kazi hiyo.

Rais Magufuli ametoa uamuzi huo katika mazungumzo yake kwa njia ya simu na Mkuu wa mkoa wa Tanga, Martine Shigela.
Rais Magufuli amesema kwamba  aliamuru kurejeshwa serikalini fedha zilizotolewa kwa ajili ya ujenzi wa jengo la Halmashauri ya Bumbuli baada ya ujenzi wa jengo hilo kutoanza kwa muda wa miaka miwili tangu fedha hizo zitolewe hivyo alitaka kuwapa wilaya nyingine zenye uhitaji .

Awali Rais Magufuli alifikia uamuzi huo baada ya viongozi wa eneo hilo kutofautiana mahali pa kujenga jengo la Halmashauri na kufanya fedha iliyotolewa na serikali kukaa bila ya kutumika kwa zaidi ya miaka miwili.

"Halmashauri ilipitisha kujengwa kwa Makao Makuu lakini watu wachache walikuwa wakipinga kwa ajili ya maslahi yao binafsi. Sisi tulitoa kama Bilioni 1.3 au 4 hivi lakini fedha zikakaa tu bila kufanya kazi. Nilitaka fedha hizo nipeleke kwenye wilaya nyingine lakini Mkuu wa Mkoa ameniomba.  Mkuu wa Mkoa amesema kwamba mnahitaji makao makuu na ofisi nzuri. Nimebadilisha maamuzi na hizo pesa zijenge makao makuu. Na siku nikija huko nitakuja kulitazama. Kuanzia sasa atafutwe Mkandarasi aanze kufanya ujenzi na pesa zikipungua mniambie nitawaongeza," Magufuli.

Pamoja na hayo Rais Magufuli amesema kuwa siasa za kubishana bishana zimepitwa na wakati kwani  Maendeleo ya Bumbuli, Lushoto na Tanga ni ya milele sisi wanasiasa ni watu wa kupita.

Naye Mkuu wa Mkuu wa mkoa wa Tanga ameahidi kutekeleza agizo hilo na kusema atawashughulikia wale wote watakaojaribu kukwamisha zoezi hilo kama ilivyokuwa awali. 

Raisi Magufuli abadili maamuzi Raisi Magufuli  abadili maamuzi   Reviewed by KUSAGANEWS on April 11, 2018 Rating: 5

No comments: