Mahakama ya Hakimu Mkazi
wa Wilaya ya Iringa inatarajiwa kusikiliza ushahidi wa anayetajwa kuwa mpenzi
wa Mwenyekiti wa Mtandao wa Wanafunzi Tanzania (TSNP), Abdul Nondo siku ya
Aprili 18.
Upande wa Jamhuri pia inakusudia
kuleta mashahidi wengine ambao ni Koplo Salum, Alphonce Mwamule, Koplo
Abdulkadir na mfanyakazi kutoka Kampuni ya Simu za Mkononi ya Tigo.
Wakili wa Serikali, Abel Mwandalamo
amesema Nondo anakabiliwa na mashtaka mawili ambayo ni kusambaza taarifa za
uongo akiwa Ubungo jijini Dar Es Salaam na kutoa taarifa za uongo akiwa mjini
Mafinga kwa askari Polisi kituo cha Mafinga Wilayani Mufindi.
Wakili Mwandalamo mbele ya Hakimu
Mkazi wa Wilaya ya Iringa John Mpitanjia, amedai upande wa Jamhuri
unakusudia kuambatanisha vielelezo vya ushahidi ambavyo ni taarifa za uchunguzi
kuhusiana na mawasiliano ya simu, maelezo kutoka Mjini Mafinga yakidai Nondo
katekwa na kuleta kielelezo cha simu za mkononi.
Hakimu Mpita Njia ameahirisha kesi
hiyo hadi Aprili 18, mwaka huu ambapo itaanza kusikilizwa kwa siku mbili
mfululizo, kutokana na maombi ya upande wa utetezi ya Wakili Charles Luoga.
Mpenzi wa Nondo kunguruma mahakamani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 11, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment