RAISI MAGUFULI AAHIDI KUSHIRIKANA NA MADHEHEBU YOTE YA DINI


Rais wa jamuhuri ya muungano wa Tanzania Dokta John Magufuli amesema mahuburi na mafundisho yanayotolea makanisani na misikitini yanarahisisha utendaji kazi wa serikali hivyo ataendelea  kushirikiana na madhehebu yote dini katika nyanja zote.

Rais Magufuli amesema hayo jana alipohudhuria ibada ya kuapishwa kwa askofu Mkuu wa Jimbo kuu  Katoliki Arusha ambapo ameeleza kuwa  madhehebu ya dini yamekuwa yakihubiri amani kwakuwa amani ni muhimu katika maisha ya kila Mtanzania hivyo ata endelea kushirikiana na madhebu yote ya dini ili kuijenga amani ya nchi.

Aidha Rais Magufuli akijibu yaliyotolewa na umoja wa mapadri wa Jimbo kuu  Katoliki Arusha  juu ya kuhamishwa kwa shule ya msingi Naura iliyopo katika eneo la kanisa,kumilikishwa bustani ya naura iliyo mbele ya kanisa hilo pamoja na kusamehewa kodi inayodaiwa  na serikali kwa shule ya st Judi inayomilikiwa na kanisa hilo amesema kuwa atakaa na serikali kuona ni yapi watanya atakama ni ushauri tuu mambo yote yapo kisheria na huwezi kutoa maamuzi yatakayoweza kuleta mgogoro katika nchi.

mhashamu askofu Mkuu wa Jimbo Katoliki Arusha ambaye ndiye aliyeapishwa Askofu Isac Amani amesema Siasa safi ni ile inayounganisha vyama vyote kuwa pamoja na kuweza kufanya kazi za maendeleo kwa kushirikiana hivyo wasirujusu ufa  utaoweza kuharibu ustawi wa nchi.

RAISI MAGUFULI AAHIDI KUSHIRIKANA NA MADHEHEBU YOTE YA DINI RAISI MAGUFULI AAHIDI KUSHIRIKANA NA MADHEHEBU YOTE YA DINI Reviewed by KUSAGANEWS on April 08, 2018 Rating: 5

No comments: