Askofu Mkuu wa Kanisa la Full
Gospel Bible Fellowship (FGBF), Zachary Kakobe amesema yeye ni raia wa
Tanzania ,"anayesema mimi si raia wa Tanzania aniambie ni raia wa nchi
gani."
Askofu Kakobe ametoa kauli hii leo
Aprili 9,2018 mara baada ya kutoka kuhojiwa kwa takriban saa tatu kuhusu
uraia wake katika Ofisi ya Uhamiaji mkoa wa Dar es Salaam
Amesema uhamiaji wanaweza kuwa na
nia njema lakini, "kwa nini sasa, kwa nini wanahojiwa watu wa aina
fulani wa kutoka eneo fulani la Kigoma. Mbona hatujasikia kutoka Dodoma,
Kaskazini wakihojiwa."
"Mimi ni Mtanzania na kama
kuna mtu anasema si raia basi aniambie mimi ni raia wa nchi gani,"
amesema Askofu Kakobe
Amesema, ametakiwa kuacha hati
yake ya kusafiria ili iweze kuwasaidia kupata taarifa zake muhimu huku yeye
akisisitiza "hiki wanachokifanya kina tia shaka
Mahojiano ya kiongozi huyo wa
kiroho yaliyoanza Saa 4.53 asubuhi hadi saa 7.55 mchana yamehitimishwa
|
Kakobe ahojiwa Uhamiaji
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 09, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment