Rais John Magufuli amesema mabadiliko
yaliyofanyika ndani ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na Mkurugenzi
wa Mashtaka (DPP) ni kuondoa changamoto ya Serikali kushindwa katika kesi mara
nyingi
Alisema hayo jana Ikulu, Dar es Salaam
wakati akiwaapisha majaji 10 wa Mahakama Kuu na Naibu Mwanasheria Mkuu wa
Serikali, Wakili Mkuu wa Serikali, Naibu Wakili Mkuu wa Serikali na Naibu
Mkurugenzi wa Mashtaka
Katika mabadiliko aliyoyafanya, Aprili 15
Rais Magufuli alimteua Dk Julius Mashamba kuwa Wakili Mkuu wa Serikali, Dk Ally
Possi (Naibu Wakili Mkuu wa Serikali) na Naibu Mkurugenzi wa Mashtaka, Edson
Makallo ambao jana aliwaapisha kuanza majukumu hayo mapya
Rais Magufuli alisema mara baada ya kuingia
madarakani Novemba 5, 2015 moja ya maswali aliyokuwa akijiuliza ni kwa nini
Serikali imekuwa ikishindwa kesi nyingi huku ikitumia wanasheria wa kampuni
binafsi
Awali, Waziri wa Katiba na Sheria, Profesa
Palamagamba Kabudi alisema mwaka 2016 akiwa mwalimu wa chuo kikuu mwenye
mkataba wa muda baada ya kuwa amestaafu, Rais Magufuli alimwita na kutaka kujua
kwa nini Serikali inashindwa kesi
Alisema katika mazungumzo hayo alimweleza
kwamba kunahitajika mabadiliko ya kimfumo katika ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa
Serikali na ile ya Mkurugenzi wa Mashtaka jambo ambalo Rais Magufuli
amefanikiwa kulitekeleza na matunda yake yataanza kuonekana
Rais Magufuli alisema tangu kufutwa kwa cheo
cha Wakili Mkuu wa Serikali miaka 40 iliyopita kilichoongozwa mara ya mwisho na
Jaji Mark Bomani, “tangia hapo, Serikali imekuwa ikishindwa kesi nyingi sana.
Kesi yenye pesa, unakuta wakili wa Serikali na mtetezi wanaungana na kuwa kitu
kimoja, kitu ambacho anatakiwa kukifanya hakifanyi hatimaye Serikali
inashindwa. Ndio maana kuna kesi tulitumia Euro milioni saba (zaidi ya Sh18.7
bilioni), kwa nini tunashindwa,” alihoji Rais Magufuli, “Kwa nini kama tuna
Mwanasheria Mkuu wa Serikali na wanasheria wazuri tunatumia kampuni za nje?
Rais Magufuli alisema, “subirini wakati wa kusikiliza kesi za uhujumu uchumi wanasheria watajaa huko.”
Kuhusu majaji, Rais Magufuli alisema kazi ya
kuwateua ni ngumu na kuwataka kumtanguliza Mungu mbele wanapotekeleza majukumu
yao ya kila siku
“Mtakutana na kesi za huruma za watoto
maskini au wajane, kwa kuwa anayemshitaki ana pesa nyingi, kamtangulizeni Mungu
mbele mnapotekeleza majukumu yenu,” alisema Rais Magufuli.
Kuhusu mabadiliko hayo DPP, Biswalo Mganga
alisema, “yataleta tija kubwa sana.”
Akizungumza kabla ya kumkaribisha Rais, Jaji
Mkuu wa Tanzania, Profesa Ibrahim Juma aliwakumbusha majaji hao dhamana
waliopewa na akawataka kuwa waadilifu na kuchapa kazi kwa bidii ili kuepuka
kuangukia mikononi mwa Tume ya Utumishi wa Mahakama.
“Katiba inawalinda lakini pia kumbukeni kama
mtakuwa na mienendo mibaya mtaanza kufuatiliwa na tume,” alisema.
Alisema kuchaguliwa kwa majaji hao
kumepunguza mzigo wa majaji kusikiliza mashauri mengi kwa mwaka. “Mzigo wa jaji
mmoja kusikiliza mashauri 535 kwa mwaka sasa unashuka hadi kufikia 460,”
alisema.
Alisema kwa kawaida jaji anatakiwa
kusikiliza mashauri 178 kwa mwaka lakini kulingana na mazingira ya Tanzania,
wastani uliowekwa ni kusikiliza mashauri 220 kwa mwaka.
Rais Magufuli azungumzia mabadiliko ofisi ya AG, DPP, awaapisha majaji 10
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 20, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment