Rais Magufuli awataka Iringa kutumia barabara ya lami


Rais John Magufuli amewataka wanakijiji cha Migori mkoani Iringa kutumia barabara ya lami ya Iringa-Dodoma kujitajirisha

Akizungumza leo Jumapili Aprili 29, aliposimama kwa muda katika kijiji cha Migori wakati akielekea Iringa, Rais Magufuli amewataka wanakijiji hao kuchapa kazi

“Barabara imekamilika mnaiona, itumieni ili mtajirike, limeni mazao kwa bidii na msafirishe kwenda sehemu mbalimbali za nchi,” amesema Rais Magufuli

Aliwataka kutumia mvua zinazoendelea, kulima na kufuga ili waweze kunufaika

Rais Magufuli atakuwa na ziara mkoani Iringa ambako Jumanne Mei mosi atakuwa mgeni rasmi katika sherehe za Siku ya Wafanyakazi Duniani zitakazofanyika kitaifa mkoani Iringa

Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Amina Masenza amesema sherehe hizo zitahudhuriwa na Makamu wa Rais, Samia Suluhu, Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, Spika wa Bunge, Job Ndugai, mawaziri na wabunge.

Rais Magufuli awataka Iringa kutumia barabara ya lami Rais Magufuli awataka Iringa kutumia barabara ya lami Reviewed by KUSAGANEWS on April 29, 2018 Rating: 5

No comments: