Kuna aina nyingi za ushujaa. Wapo mashujaa wa vita, ukombozi
wa kisiasa na wengine ni mashujaa wa harakati za kupambana na mambo yasiyofaa
katika jamii
Mwanafunzi Rehema John (siyo jina halisi), aliyehitimu
darasa la saba mwaka jana katika Shule ya Msingi Kasamwa wilayani Geita na
kufaulu akitakiwa kujiunga na Sekondari ya Kasamwa ni miongoni mwa walioingia
kwenye orodha ya mashujaa mwaka huu.
Ushujaa
wa binti huyo mwenye miaka 13 ni kupambana na kufanikiwa kuzuia mpango wa
wazazi na ndugu zake kumuoza kwa mwanaume aliyemlipia mahari ya ng’ombe watano
na Sh100,000 tangu akiwa shuleni.
Hii
ni baada ya kufanikiwa kumtoroka mwanaume huyo siku moja baada ya kukabidhiwa
kwake na kulala naye usiku kucha kutokana na kuogopa giza nene iliyokuwa
imetanda nje.
Pia, jitihada hizo
zimefanikisha baba yake mzazi, Kashilimu Mashimba (60), dada yake, Kefline
Mashimu na ‘mumewe’ Sayai Petro, wakazi wa Kasamwa mjini Geita kutiwa mbaroni
na polisi.
Kamanda wa polisi Mkoa wa
Geita, Mponjoli Mwabulambo aliliambia gazeti hili kuwa watuhumiwa hao
wanashikiliwa tangu Aprili 27.
Alisema
bila kujua mpango wa wazazi na dada yake, Machi 14 mwananfunzi huyo alitakiwa
kujiandaa kwenda kwa mume wake ambaye tayari ilikuwa amelipa mahari hayo.
“Mahari
ya kumuoa yalitolewa na baba wa Sayai anaitwa Petro Masalu ambaye pia ni
miongoni mwa watakaokabiliana na mkono wa sheria,” alisema.
Mwanafunzi
huyo alilieleza gazeti hili: “Usiku ule sikuwa na namna ya kutoroka kwa kuogopa
giza nene, kulipopambazuka nilidanganya kuwa naenda dukani nikapata upenyo wa
kukimbilia kwa marafiki wa elimu waliokuwa wakifika shuleni kutuelimisha
umuhimu wa shule na namna ya kukabiliana na ndoa za utotoni,” alisema
Rehema.
Mwanafunzi awadakisha baba, dada
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 30, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 30, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment