Mtoto mmoja afariki dunia, wawili walazwa baada ya kula chakula chenye sumu.


Mtoto wa miaka minne, Ashraf Hussein Hamad amefariki dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Wete, Mkoa wa Kaskazini Pemba ikidaiwa alikula chakula chenye sumu

Kamanda wa polisi Kaskazini Pemba, Haji Khamis Haji amethibitisha kupokea taarifa za kifo hicho na wengine wawili waliolazwa hospitalini baada ya kula chakula chenye sumu

Naye daktari wa zamu wodi ya watoto katika hospitali hiyo, Dk Badru Ali Badru alisema tukio hilo lilitokea juzi

Dk Badru alisema mtoto huyo na wenzake wawili walifikishwa hospitalini hapo wakiwa na maumivu makali ya tumbo

Aliwata wanapata huduma kuwa ni Akram Mohamed (6) na Mula Omar (4) ambao afya zao zinaendelea kuimarika.
Mtoto mmoja afariki dunia, wawili walazwa baada ya kula chakula chenye sumu. Mtoto mmoja afariki dunia, wawili walazwa baada ya kula chakula chenye sumu. Reviewed by KUSAGANEWS on April 30, 2018 Rating: 5

No comments: