Mtanzania Kema Salum amepandishwa kwa mara
ya kwanza kizimbani katika Mahakama ya Crown kwa tuhuma za kumuua mke wake,
Leyla Mtumwa
Salum (38) anadaiwa kumuua mke wake, Leyla,
Ijumaa ya wiki iliyopita kwa kumchoma visu mara kadhaa shingoni na kifuani.
Mauaji hayo yalifanyika nyumbani kwa wanandoa hao, Kirkstall Avenue, Haringey,
Uingereza
Leyla, ni mtoto wa Hidaya Mtumwa,
mwanamke aliyewahi kutungiwa wimbo na mwanamuziki wa Jamhuri ya Demokrasia ya
Congo, Pepe Kale, miaka ya 90
Hata hivyo, kesi ya Salum haikuweza
kusikilizwa baada ya kuwepo kwa mgomo wa wanasheria wa ngazi za juu nchini humo
ulioanza tangu Aprili Mosi, mwaka huu
Wakili wake, Seona White amesema
amewasiliana na vitengo zaidi ya 20 vya wanasheria, lakini hakuna aliyekubali
kumtetea Salum kutokana na mgomo unaoendelea
“Sijui hali hii itaendelea kwa muda gani
lakini natumaini mgogoro utatatuliwa haraka,” amesema
Jaji wa mahakama hiyo, Anuja Dhir amesema
kesi hiyo itasikilizwa tena Juni 20 na akaamuru mtuhumiwa arudishwe mahabusu
Jaji Dhir amesema mbele ya mahakama hiyo
kuwa, licha ya Salum kukosa wakili wa kumtetea mahakamani, lakini mwanasheria
wake hana budi kuhakikisha anapata haki zake msingi kwani si makosa yake
Salum alitafsiriwa lugha ya Kiingereza na
mkalimani mahakamani hapo
Mtanzania aliyemuua mkewe apandishwa kizimbani Uingereza
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 05, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment