Makosa matatu ya Heche haya hapa

Mbunge wa Tarime vijijini, John Heche ameunganishwa katika kesi inayowakabili viongozi saba wa Chadema na kusomewa mashtaka matatu ikiwamo kuchochea chuki

Washtakiwa wengine katika kesi hiyo ya jinai namba 112 ya 2018 ni Mwenyekiti wa Chadema, Taifa, Freeman Mbowe, Mbunge wa Iringa Mjini Peter Msigwa na Naibu Katibu Mkuu Zanzibar Salum Mwalimu

Wengine ni Naibu katibu Mkuu bara, John Mnyika, Mbunge wa Tarime mjini Ester Matiko, Katibu wa chama hicho Dk Vincent Mashinji na Halima Mdee Mbunge wa Kawe

Hata hivyo baada ya kusomewa mashtaka hayo Heche alifanikiwa kupata dhama

Akimsomea mashtaka, Heche, Wakili wa Serikali Mkuu Faraja nchimbi alidai kuwa Heche na wenzake hao saba kwa pamoja walitenda makosa hayo Februari 16, 2018 maeneo ya Viwanja vya Buibui na barabara ya Kawawa wilayani Kinondoni, Dar es Salaam
shtaka la kwanza Heche anadaiwa kufanya mkusanyiko usio halali kinyume na sheria, katika barabara ya Kawawa Mkwajuni wilayani Kinondoni Dar es Salaam, Februari 16.

Shtaka la pili ni kuendelea kufanya mkusanyiko usio halali, licha ya kutakiwa kuondoka eneo hilo na Ofisa polis Gerald Ngiichi na hivyo kusababisha kifo cha Akwilina Akwilini. Huku askari wawili wakijeruhiwa katika mkusanyiko huo.
Shtaka la  tatu,   linamkabili Heche peke yake ambapo,  anadaiwa kuwa Februari 16, mwaka huu katika viwanja vya Buibui wilayani Kinondoni, Dar es Salaam, alihutubia  katika mkutano wa hadhara  na alitamka maneno yenye kuchochea chuki  akisema

“Kesho patachimbika, upumbavu unaofanywa kwenye nchi hii...wizi...unaofanywa na Serikali ya awamu ya tano...watu wanapotea...watu wanauawa wanaokotwa kwenye mitaro lazima ukome."
Nchimbi alidai kuwa maneno hayo yalielekea kuleta chuki na manung'uniko miongoni mwa jamii na wakazi  wa Tanzania
Baada ya kusomewa mashtaka hayo, Heche alikana na Aprili 16, 2018 yeye na wenzake saba watasomewa maelezo ya awali mahakamani hapo
Heche aliachiwa kwa dhamana baada ya kukamilisha masharti ya dhamana, ya kuwa na wadhamini wawili wenye barua za viongozi wa mtaa, vijiji ama waajiri wao na nakala za vitambulisho vyao.
Kama ilivyokuwa kwa kina Mbowe, wadhamini hao kila mmoja atasaini bondi ya Sh 20 milioni na mshtakiwa kuripoti polisi kila Alhamisi.
Makosa matatu ya Heche haya hapa Makosa matatu ya Heche haya hapa Reviewed by KUSAGANEWS on April 05, 2018 Rating: 5

No comments: