Mbowe ampongeza Fatma Karume

Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amempongeza Rais mpya wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Fatma Karume huku akisema chama hicho kitampa ushirikiano wa kutosha

Taarifa kwa umma iliyotolewa leo Aprili 15, 2018 na Mbowe ambaye pia ni Kiongozi wa Kambi Rasmi ya Upinzani bungeni amewapongeza viongozi wengine waliochaguliwa sambamba na Fatma akisema, “kukuchagua kuwa rais wa chama chao katika kipindi ambacho Taifa linamhitaji mtu jasiri, makini na shupavu kama wewe

“Ushindi wako umetuma ujumbe kuwa mawakili wa Tanganyika wanajua msimamo wako na wanaamini kwa dhati kuwa kwa kushirikiana na viongozi wenzako mliochaguliwa kuongoza TLS utawavusha katika kipindi hiki ambacho Taifa linapitia na kushuhudia majaribu mengi ya uvunjifu wa Katiba, sheria na kanuni mbalimbali.”
Mbowe amesema, “umepokea kijiti katika wakati ambao mtangulizi wako (Tundu Lissu) yuko hospitalini baada ya jaribio la shambulizi lililolenga kumuua kushindikana.”
huyo ameendelea kusema, “tukutie moyo kuwa Chadema kama taasisi ya kisiasa tukiwa wadau wa masuala ya haki, sheria na utawala bora tuko nawe na tutaendelea kukupa ushirikiano wakati wote wa uongozi wako, wewe na wenzako wote.”
Amesema wanampongeza kwa kuweka historia ndani ya Taifa kwa kuwa mwanamke wa pili kushika wadhifa huo mkubwa kuongoza TLS
Fatma alichaguliwa jana kuwa rais wa TLS katika mkutano mkuu wa mawakili uliofanyika mjini Arusha akichukua nafasi iliyoachwa wazi na Lissu.
Mbowe ampongeza Fatma Karume Mbowe ampongeza Fatma Karume Reviewed by KUSAGANEWS on April 15, 2018 Rating: 5

No comments: