Masogange awakutanisha Kiba na Mond


Wasanii maarufu wa muziki wa Bongo Fleva, Diamond Platnumz na Ali Kiba wamekutana katika msiba wa Agnes Masogange na kusalimiana

Mara baada ya wasanii hao kusalimiana kwa kupeana mikono wakiwa katika meza kuu, waombolezaji waliojaa kwenye Viwanja vya Leaders walipiga kelele.

Diamond alimsalimia Kiba kwa kumpa mkono,baada ya tukio hilo, MC Pilipili alisikika akisema: “Unaona sasa, hawana ugomvi hawa.”

Kumekuwa na taarifa za wanamuziki hao kuwa na ugomvi kwa muda mrefu ambao hata hivyo, unatajwa kutengenezwa na mashabiki wao wa ‘Team Kiba na Team Diamond.’

                                                      
Masogange awakutanisha Kiba na Mond Masogange awakutanisha Kiba na Mond Reviewed by KUSAGANEWS on April 22, 2018 Rating: 5

No comments: