Makamu wa Rais kumwakilisha JPM Uingereza


Makamu wa Rais, Samia Suluhu Hassan anaondoka leo Aprili 15, 2018 
kwenda jijini London nchini Uingereza kumwakilisha Rais John Magufuli 
katika mkutano wa wakuu wa nchi za Jumuiya ya Madola (CHOGM
 
Mkutano huo utafanyika kuanza kesho, Aprili 16 hadi 20 na 
utafunguliwa na Mkuu wa Jumuiya ya Madola, Malkia Elizabeth wa 
Pili wa Uingereza ukiwa na kaulimbiu inayosema, “Kuelekea 
mustakabali wa pamoja” na  utaongozwa Waziri Mkuu wa Uingereza, 
Theresa May atakayekuwa mwenyekiti.
 
Taarifa iliyotolewa leo na ofisi ya Makamu wa Rais imesema 
majadiliano ya mkutano huo yatajikita kwenye maeneo manne 
makuu ya kipaumbele ambayo yatajadili namna ambavyo Jumuiya ya 
Madola inaweza kufikia mustakabali wenye ustawi zaidi; mustakabali 
endelevu zaidi; mustakabali wenye haki zaidi na mustakabali wenye 
usawa zaidi
 
“Mijadala katika maeneo hayo ya kipaumbele itahusisha masuala 
mbalimbali ikiwemo kukuza zaidi biashara na uwekezaji baina ya nchi
 za Jumuiya ya Madola kwa manufaa ya nchi wanachama na Jumuiya 
nzima
 
Pia, kukuza na kuendeleza misingi ya demokrasia, ajenda ya 
mabadiliko ya tabia nchi na maendeleo endelevu pamoja pamoja na 
masuala ya uhalifu wa kimataifa kama vile ugaidi, uhalifu wa 
kimtandao na usafirishaji wa binadamu
 
Taarifa hiyo imeeleza kuwa, Makamu wa Rais amembana na Waziri 
wa Mambo ya Nje, Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Kikanda na 
Kimataifa, Dk Augustine Mahiga pamoja na viongozi wengine 
waandamizi kutoka wizara hiyo ambapo msafara huo unatarajia 
kurejea nchini Aprili 22.
Makamu wa Rais kumwakilisha JPM Uingereza Makamu wa Rais kumwakilisha JPM Uingereza Reviewed by KUSAGANEWS on April 15, 2018 Rating: 5

No comments: