Kesi ya Bilionea Msuya kuendelea kesho


Kesi ya mauaji ya kukusudia ya mfanyabiashara tajiri wa madini,  Erasto Msuya ambayo iliahirishwa Februari mwaka huu kwa kukosekana mashahidi, imepangwa kuendelea kusikilizwa kesho Aprili 16

Kuanzia Februari 20 hadi 23, upande wa mashtaka ulikuwa ukiomba kesi iahirishwe kwa kuwa walikuwa hawana shahidi licha ya kuiambia mahakama kuwa wana jumla ya mashahidi

Wakati jopo la mawakili wa Serikali linaloongozwa na Wakili wa Serikali Mkuu, Peter Maugo likijikuta katika sintofahamu hiyo, upande wa mashtaka ulikuwa umefanikiwa kuita mashahidi 25 kati ya 50

Februari 21, 22 na 23, Wakili Maugo anayesaidiana na mawakili waandamizi Abdalah Chavula, Omary Kibwana na Kassim Nassir alijikuta katika kibarua kigumu cha kuiomba mahakama kwa siku tatu mfululizo iahirishe kesi hiyo kwa tatizo hilo

Wakili Majura Magafu ambaye ni miongoni mwa mawakili wanne wanaowatetea washtakiwa alikaririwa kipindi hicho akisema wamesikia shida wanayopata upande wa mashtaka katika kuleta mashahidi, lakini akaomba wajitahidi ili wapatikane

“Tumesikia concern (ombi) yao lakini tunaomba wajitahidi kuhakikisha wanapatikana kwa sababu record (kumbukumbu) zao na anuani zao zipo na wanafahamika,” alisema Magafu

Mauaji ya mfanyabiashara huyo yalifanyika Agosti 7, 2013

Kesi hiyo inayovuta hisia za wengi inawakabili washtakiwa saba ambao ni Sharifu Mohamed, Shaibu Jumanne, Mussa Mangu, Jalila Zuberi, Karim Kihundwa, Sadick Jabir na Ally Mussa
Kesi ya Bilionea Msuya kuendelea kesho Kesi ya Bilionea Msuya kuendelea kesho Reviewed by KUSAGANEWS on April 15, 2018 Rating: 5

No comments: