KUNDI LA FRIENDS OF BATULI TUENDELEE KUIGUSA JAMII INAYOISHI MAZINGIRA MAGUMU KWA KADRI WANAVYOBARIKIWA



Msemaji wa kundi la Friends of batuli akikabidhi uniform za wanafunzi kwa mmoja wa walimu ambazo zimetolewa na kundi hilo katika shule ya Msingi ungalimitedi  jijini Arusha Picha Na Alphonce Kusaga



Mmoja wa wanafunzi anayeishi mazingira magumu akifurahia msaada alioupata kutoka kundi la Friends of batuli katika shule ya msingi Salei kata Ungalimitedi jiji la Arusha 
 
 Mwalimu mkuu wa shule ya msingi Salei Niminini kahema akipokea msaada kutoka kwa wadau wa kundi la Friens Of Batuli kwa ajili ya kukabidhi watoto wa shule hiyo wenye mazingira magumu

Katibu wa kundi la friends of Batuli Tausi Swalehe pamoja na msemaji wake Batuli Kisaya na mmoja wa mdau wa kundi hilo wakikabidhi msaada shule ya msingi Ungalimitedi.
Jamii imetakiwa kuthamini na kuwa karibu na makundi maalum kwa kuonyesha upendo ,faraja pamoja na ushirikiano ili makundi hayo wajisikie kama watu wengine ambao hawana matatizo.

Hayo yamesemwa na Msemaji wa kundi la Friends Of Batuli Bi Batuli Kisaya wakati wakikabidhi misaada ya Nguo za Shule,Chakula pamoja na vifaa vya Shule katika shule za msingi Ungalimitedi na Salei zilizopo katika kata ya Ungalimitedi katika halmashauri ya jiji la Arusha ambapo amesisitiza kuwa jamii ina nafasi ya kubadilisha maisha ya makundi maalum.

Batuli amesema kuwa kundi hilo limekuwa wahamasishaji wakubwa katika kufikia makundi maalum licha ya kuwa hawana vitu vikubwa vya kutoa lakini wanatoa kadri ya walivyobarikiwa na mwenyezi Mungu.

Amesema kuwa wametoa vitu mbalimbali kama vile Mafuta ya kupikia ,mchele,Nguo za shule,madaftari ,Soksi ,masweta ya Shule,sukari ,sabuni na vitu vingine jumla vina thamani ya shilingi Milioni moja.

Batuli ameongeza kuwa amesema kuwa hakuna jambo linaloshindikana endapo jamii itaamua kusaidia makundi maalum ambapo mpaka sasa wameshatoa msaada kwenye vituo vyenye makundi maalum zaidi ya 35 licha ya kuwa hawana chanzo cha mapato.

Hata hivyo makamu mwenyekiti wa kundi hilo la Friends of Batuli Bwana Aly bwanga amesema jamii inatakiwa kuwa mstari wa mbele kutambua jamii yenye uhitaji maalum kwasababu hazikupenda kuishi hivyo ambavyo wanaishi kwasasa.

Bwanga amesisitiza kuwa kila mtu anapokaa katika maeneo yanayomzunguka kuna watu wanahitaji msaada kupitia yeye kwa kuguswa kutoa kitu hata kikiwa kidogo.

Akizungumza baada ya Kupata misaada hiyo mwalimu mkuu wa shule ya Ungalimitedi Emanuel Kileo amesema katika shule hiyo kuna watoto zaidi ya 400 ambao ni yatima na wanaoishi katika mazingira magumu ambao wanahitaji msaada kutoka kwa wadau ikiwemo kundi la Friends Of Batuli.

Naye mwalimu mkuu wa shule ya msingi Salei Niminini kahema ameshukuru kundi hilo la Friends of batuli huku akiitaka jamii kutoa msaada kila wakati bila kusubiri kipindi maalum kama kwenye sikuu za mfungo wa ramadhani ,sherehe za kidini pamoja na sherehe malum.

“Mimi nafikiri tusitegemee siku za Special Days iwe mwaka mzima kwamba hizi kazi zifanyike mwaka mzima kwasababu mahitaji ya watoto hayategemei siku za siku kuu tu mwaka mzima hawa watoto wana shida tunajitoa hata sisi kama walimu kuna wengine hawana viatu hawana nguo za shule ,viatu yani hawana kabisa kitu hiki kitendeke mwaka mzima unapobarikiwa toa tusisubiri hizo siku kuu mara nyingi wengi wanasubiria Idi ,na Krismas Jamani shida hazina Krismas tuna jambo la kuiga kutoa kwenu friends of batuli”Mw/mkuu shule ya Salei Niminini Kahema

Kwa upande wa Shekhe wa wilaya ya Arusha Dc Shekh Hussein Saidi Ijunje amesema kuwa wanachokifanya kundi la Friends of Batuli ni jambo ambalo linatakiwa kuigwa na kila mmoja katika jamii kwa kuwa hata maandiko matakatifu yamelekeza kusaidia makundi maalum.

Shekh Hussein amesema makundi mbalimbali ambayo yapo yaige mfano wa kundi hilo kwa kuhakikisha wanatenga kitu kidogo kwa ajili ya kusaidia makundi yenye mahitaji maalum.

Licha ya kutembelea shule Mbili za msingi Ungalimitedi pamoja na shule Salei pia wametembelea kituo cha CHISEA kilichopo kata ya ungalimitedi jijini Arusha ambapo kituo hicho wameshukuru kwa msaada wa kutoka kwa kundi hilo









KUNDI LA FRIENDS OF BATULI TUENDELEE KUIGUSA JAMII INAYOISHI MAZINGIRA MAGUMU KWA KADRI WANAVYOBARIKIWA KUNDI LA FRIENDS OF BATULI TUENDELEE  KUIGUSA JAMII INAYOISHI MAZINGIRA MAGUMU KWA KADRI WANAVYOBARIKIWA Reviewed by KUSAGANEWS on April 21, 2018 Rating: 5

No comments: