|
Uongozi wa Serikali na Polisi mkoani
Mara, wanafanya mashauriano na familia ya Suguta Marwa, ndugu wa mbunge wa
Tarime Vijijini (Chadema), John Heche anayedaiwa kuuawa na polisi kwa
kuchomwa kisu usiku wa kuamkia Aprili 27
Majadiliano hayo yanaendelea huku
kamanda wa polisi Kanda Maalumu Tarime/Rorya, Henry Mwaibambe
akitangaza askari anayetuhumiwa kufanya mauaji hayo, E.1156 Koplo William
Marwa kushikiliwa kwa mahojiano
Mkuu wa Mkoa wa Mara, Adam Malima
juzi Aprili 27, 2018 alitembelea familia ya marehemu na kuahidi kuwa Serikali
itahakikisha hatua za kisheria zinachukuliwa ili haki itendeke
“Hakuna mtu aliye juu ya sheria
hata ningekuwa mimi Adam Malima, mkuu wa mkoa ndiye ningefanya jambo hili
ningechukuliwa hatua za kisheria. Haki ya marehemu lazima ipatikane,” amesema
Malima
Licha ya kuitembelea familia
kuhani msiba akiwa ameongoza na wajumbe wa kamati ya ulinzi na usalama ya
mkoa, Malima alitembelea Kituo cha Polisi Sirari na chumba cha kuhifadhi
maiti cha Hospitali ya Wilaya ya Tarime ulikohifadhiwa mwili wa Suguta tangu
juzi
Msemaji wa familia, Philemon
Suguta amesema vikao kati yao na Serikali kuhusu msiba huo vitafanyika baada
ya baadhi ya ndugu akiwamo mbunge Heche ambao wapo njia kwenda Tarime
kuwasili
“Jambo la msingi kwa familia ni
hatua za kisheria kuchukuliwa, haiwezekani mtuhumiwa aliyekamatwa akiwa hai
afie mikononi mwa polisi, tena kwa kuchomwa kisu,” amesema Suguta
Baba mgogo wa marehemu, Issa
Suguta aliwatuhumu polisi waliomkamata ndugu yake kumpiga hadi kumjeruhi
kabla ya kummalizia kwa kumchoma kisu
Naye katibu wa Chadema mkoa wa
Mara, Chacha Heche ambaye ni ndugu wa marehemu Suguta amesema hadi sasa,
familia inaamini mauaji hayo ni uhalifu usiohusiana na masuala ya kisiasa
|
|
Kifo mdogo wa Heche ngoma nzito
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 29, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 29, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment