Rais John Magufuli amefika Iringa na
kusimulia mara ya kwanza alipopelekwa mkoani humo kusoma kwamba hakula nyama
kwa mwezi mmoja baada ya kutahadharishwa na watu kuwa akifika asile kitoweo
hicho.
Akihutubia wakazi wa Iringa wakati wa
ufunguzi wa barabara ya Iringa-Fufu leo Aprili 29, 2018; Rais Magufuli amesema
alifika Iringa kwa mara ya kwanza mwaka 1978/79 kwa ajili ya masomo katika
Sekondari ya Mkwawa
“Niliambiwa usile nyama, usile mshikaki
Iringa na kweli sikula," amsema na kwamba, baada ya kukaa muda alibaini
wakazi wa Iringa hasa wanaume kuwa ni wakarimu
"Wanaume wa Iringa ni wapole sana,
unamchokoza lakini anajinyonga yeye badala ya kukuadhibu wewe," ameongeza
Rais Magufuli huku akishangiliwa na umati wa wananchi
Anasema watu wa Iringa ni tofauti na wenzao
wa mkoani Mara ambao ukiwachokoza utakiona cha mtema kuni
Rais Magufuli asema hakula nyama mwezi mmoja akiwa Iringa
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 29, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 29, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment