Wazazi wawili wenye dini
ya Kiislam nchini Ufaransa wamepelekwa mahakamani baada ya kumpa mtoto wao jina
la 'Jihad' na kujaribu kulisajili rasmi serikalini.
Maafisa wa serikali wa Ufaransa
baada ya taarifa hiyo waliamua kuwafikisha kwa waendesha mashtaka, ambao sasa
hivi wanaendesha kesi hiyo kupingana nalo wakiamini kuwa jina hilo lina
muunganiko na ugaidi.
Wazazi hao walijaribu kujitetea kwa
kuwaeleza waendesha mashtaka kwamba jina hilo halina maana ya vita vitakatifu
kama ambavyo wengi wanafahamu, bali ni nguvu na kuweza kujipigania.
Hata hivyo maafisa wa serikali wa
Ufaransa wamesema wamewataka wazazi hao kubadili jina la mtoto huyo ili
kumlinda na madhara yake baadaye, na wazazi hao kufikia muafaka hapo jana April
16, 2018, na kumuita Jahid.
Nchini Ufaransa mzazi ana uhuru wa
kumpa mtoto jina lolote analopenda, lakini lisiwe na madhara kwenye maisha ya
mtoto huyo kwa namna yoyote ile.
Jina la mtoto lawafikisha wazazi mahakamani
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 17, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment