BREAKING NEWS: FATMA KARUME ASHINDA URAIS WA TANGANYIKA LAW SOCIETY (TLS)


Mwanasheria mkongwe, Fatma Karume, ameshinda nafasi ya urais wa Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS

Fatma, ambaye licha ya kuwa mwanachama wa TLS kwa muda mrefu, lakini pia ni mtoto wa Rais wa sita wa Zanzibar, Amani Abeid Karume

Zoezi la kupiga na kuhesabu kura lilianza tangu asubuhi leo Aprili 14, mjini Arusha na likakamilika jioni huku Fatma akiibuka na kura  820 dhidi ya mpinzani wake wa karibu, Wakili Godwin Ngwilimi, aliyepata kura 363

Wagombea wengine wa nafasi ya urais wa TLS walikuwa ni Godwin Mwapongo aliyepata kura 12 na Godfrey Wasonga, aliyepata kura sita

Fatma Karume amezaliwa Juni 15, 1969, visiwani Zanzibar, 

Ni Mtoto wa rais wa sita wa Zanzibar, Amani Abeid Karume

Ni mjukuu wa Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Abeid Amani Karume

Ni mwanasheria katika kampuni ya uwakili ya IMMA Advocates

Ni mwanzilishi wa kampuni ya uwakili ya Karume and Co Advocates 2004

Fatma amewahi kuwa mwanasheria wa mwanasiasa Tundu Lissu katika kesi yake ya uchochezi, Julai mwaka jana

Ofisi za kampuni ya uwakili ya IMMMA zilizopo Upanga, jijini hapa, ziliungua moto Agosti mwaka jana




BREAKING NEWS: FATMA KARUME ASHINDA URAIS WA TANGANYIKA LAW SOCIETY (TLS) BREAKING NEWS: FATMA KARUME ASHINDA URAIS WA TANGANYIKA LAW SOCIETY (TLS) Reviewed by KUSAGANEWS on April 14, 2018 Rating: 5

No comments: