Gerald Waya,
ambaye ni baba mzazi wa Agnes (Masogange), amesema mwanaye alikuwa nguzo katika
maisha yake, hivyo ni pigo kubwa kwake na familia nzima
Waya
akizungumza nyumbani kwake Mbalizi II wilayani Mbeya, leo Aprili 22, 2018
amesema Masogange ni mtoto wanne katika familia yake ya watoto sita, wa kike
wakiwa watano.
Amesema
Masogange alisoma Shule ya Msingi Utengule-Mbalizi na sekondari ya Sangu
alikoishia kidato cha pili.
Waya amesema Masogange alipata matatizo hivyo
akalazimika kuacha shule. Hata hivyo amesema hataki kuzungumzia mambo mabaya
wakati huu anapoomboleza kifo cha mwanaye
“Aliishia form
two (kidato cha pili), akapata matatizo ikabidi aache shule. Tulikosana
kidogo lakini tukayamaliza yeye akaenda Dar es Salaam,” amesema
Waya amesema,
“Mwanangu alikuwa nguvu kwangu, alikarabati nyumba hii ninayoishi kwa sasa na
nilikuwa nafarijika sana, lakini leo kusikia msiba huu kwa kweli inaniuma
sana.”
Amesema
Masogange alimpigia simu, “Tukaongea naye akaniambia ‘mimi baba ninaumwa’.
Nikamuuliza nini tatizo akasema, “aah! baba niombee tu kwa Mungu’.
Na Jumamosi iliyopita nilimpigia simu wakati yupo hospitali kujua maendeleo
yake lakini akaniambia ‘baba byee’. Nikaanza kulia, na hapo sikuwasiliana
naye tena hadi nilipopata taarifa za kifo chake,” amesema.
Baba mzazi wa Masogagnge asimulia siku za mwisho ya mwanae
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 22, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment