Askofu Mkuu wa Jimbo kuu Katoliki la Arusha,
Isaac Amani, Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro, Anna Mghwira na Mkuu wa Wilaya ya
Same, Rosemary Senyamule jana walishiriki katika ibada ya mazishi ya mapadri
watatu waliofariki mfululizo kwa matukio tofauti
Mapadri hao, Ulbadius Kidavuri, Arbogast
Mndeme na Michael Kiraghenja walizikwa jana katika makaburi ya mapadri,
yaliyopo Chanjale, wilayani Mwanga
Akizungumza katika ibada hiyo, Askofu Mkuu
mstaafu wa Jimbo Kuu Katoliki Arusha, Josephat Lebulu alieleza jinsi
alivyopokea kwa mshtuko taarifa za vifo hivyo vilivyotokea mfululizo
Hata hivyo, aliwaambiwa waombolezaji kuwa,
“Tunajua yaliyotokea yanauma sana hivyo kuweni na matumaini.”
Aliwataka waumini kuomboleza na kulia kwa
matumaini
“Nilipompigia simu ndugu yangu Askofu Rogath
Kimario (wa Jimbo Katoliki Same) kumpa pole kuhusiana na kifo cha Padri
Kiraghenja, aliniambia kuna msiba mwingine umetokea wa pili wa Padri Mndeme
ambaye alifariki dunia April 12. Akanambia unafikiri ni vifo hivyo tu, kuna
msiba mwingine tena wa Padri Kidavuri uliotokea Kurasini Dar es Salaam. Kwa
kweli nilisikitika sana,” alisema akisimulia jinsi alivyopoata taarifa za vifo
hivyo
Katika salamu zake za pole, Mghwira alisema
vifo vya mapadri hao ni pigo kubwa kwa jimbo hilo kwani ni watumishi ambao
walikuwa wakitegemewa na jamii
“Kwetu ni pigo kubwa kuwapoteza mapadri
watatu kwa mpigo. Hawa ni viongozi wa kijamii ambao tunawahitaji sana katika
jamii zetu,” alisema Mghwira
Kuhusu vifo vya mapadri hao
Padri Kiraghenja alikuwa Paroko wa Kanisa la
Kirangare, Moshi na alifariki dunia Aprili 11 baada ya kujisikia vibaya, kisha
kunywa dawa ya maumivu. Alifariki akiwa usingizini
Padri Mndeme alikuwa katika Parokia ya
Lembeni, Mwanga. Alifariki dunia Aprili 13 akiwa kwenye uchunguzi wa matibabu
Hospitali ya KCMC baada ya kufanyiwa upasuaji wa kuondoa uvimbe wa saratani ya
utumbo mpana
Padri Kidavuri alikuwa Katibu Mtendaji wa
Utume wa Walei katika Baraza la Maaskofu Tanzania (TEC). Alifariki dunia Aprili
13 kwa shinikizo la damu baada ya kupata taarifa za vifo vya wenzake
Askofu Lebulu, Mghwira watoa neno mazishi ya mapadri watatu Mwanga
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 18, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment