Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey
Polepole amedai kuwa Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe hajui hesabu kwa kuwa
hakuna fedha iliyopotea hivyo amemshauri amtafute mtaalam wa hesabu
Polepole amesema hayo leo Jumatano Aprili 18
alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu ripoti ya Mdhibiti na
Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali(CAG
Polepole amesema, “Huyu ni muongo alianza na
santuri ya njaa akatangaza nchi ina njaa. Tumezunguka nchi nzima hakuna njaa,
akaona haitoshi akamgeukia rais wetu kuwa ni dikteta wakati yeye anaendesha
chama kupitia Facebook.”
“Kuna wakati anasema kamati kuu imekaa kumbe
uongo anaandika facebook”
“Niombe
uongozi wa Bunge wakati mwingine uwe unawabana wabunge wawe wanathibitisha
mambo wanayoyazungumza bungeni.”
“Wenye dhamana ya kusimamia sheria wachukue
hatua, kucheka cheka na mizaha kwa kauli hizi haivumiliki. Tunataka aeleze hiyo
Sh 1.5 trilioni kaipata wapi, alizua taharuki, nasisitiza tusimuache alizoeshwa
vibaya huyu maana tunajua sisi ndio tupo kwenye chama.”
Baada ya Polepole kueleza hayo Zitto amejibu
katika mitandao ya kijamii akieleza, “Kuna mtu anasema nikamatwe kwa kupotosha
kuhusu TZS 1.5trilioni zinazohojiwa na CAG”
“Nipo tayari kukamatwa kwa kusema hivyo
(haitafuta ukweli wa ubadhirifu huo).”Chama cha Mapinduzi(CCM) kimesema kuwa kuna viongozi wa upinzani
wamekuwa wakitoa taarifa za uongo kuupotosha umma, tabia ambayo haikubaliki,
haivumiliki na itafika wakati watasema sheria ichukue mkondo wake maana
wanaleta taharuki kwa wananchi
ZITO KABWE AMJIBU POLEPOLE KUWA YUKO TAYARI KUKAMATWA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 18, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment