Chama cha Mapinduzi(CCM) kimesema kuwa kuna
viongozi wa upinzani wamekuwa wakitoa taarifa za uongo kuupotosha umma, tabia
ambayo haikubaliki, haivumiliki na itafika wakati watasema sheria ichukue
mkondo wake maana wanaleta taharuki kwa wananchi
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Hamphrey
Polepole amesema hayo leo Jumatano Aprili 18 wakati akifafanua mambo kadhaa
yanayopotoshwa katika Ripoti ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za
Serikali(CAG
Polepole amesema imekuwa tabia na mtaji wa
kiongozi huyo ambaye hakumtaja jina kutoa taarifa za uongo
“Kiongozi unasema fedha zimeibiwa sijiu
akiambiwa atoe ushahidi atasemaje. Siku hizi hana hoja ana kazi ya kuleta
taharuki kwa umma,” amesema Polepole
“Hatuko tayari kuendelea kuona watu wachache
wauhadaa umma.”
Amesema CCM hakiamini malumbano, mabishano
yasiyo na tija, lugha za kubeza, kebehi na kufifisha moyo wa kizalendo kwa
Watanzania
“Nchi yetu ina mfumo wa kidemokrasia ya
vyama vingi lakini CCM inaendelea kuamini sisi ni wamoja.”
CCM yaja juu viongozi wa upinzani wanaodaiwa kupotosha ripoti ya CAG
Reviewed by KUSAGANEWS
on
April 18, 2018
Rating:
No comments:
Post a Comment