AFISA WA POLISI AHUKUMI WA MIAKA 15 JELA KWA KUFANYA MAUAJI


AFISA wa Polisi aliyejipatia sifa lukuki kwa kupunguza uhalifu katika eneo la Githurai, Ruiru, kaunti ya Kiambu mwaka mitano iliyopita amehukukumiwa kifungo cha miaka 15 jela kwa mauaji.
Titus Ngamau Musila almaarufu Katitu alisukumiwa miaka hiyo na Jaji James Wakiaga aliyempata na hatia ya kumuua Kennedy Kimani Mwangi kwa kumpiga risasi Machi 4, 2013, katika steji ya Githurai 45.

Kati ya miaka hiyo 15 Katitu atatumikia mitatu kifungo cha nje.
Miaka itakayosalia 12 atakuwa gerezani.

Pia Jaji James Wakiaga aliyempata Katitu Februari 7, 2018, na hatia ya kumuua Kimani alisema miaka minne ambayo mshtakiwa alikuwa rumande itazingatiwa na idara ya magereza ndipo itolewe katika kifungo hicho cha miaka 12.

Hivyo basi Katitu atatumikia kifungo cha miaka minane jela ndipo atoke atumikie kifungo cha miaka mitatu chini ya uangalizi wa Afisa wa urekebishaji tabia.

Akipitisha hukumu, Jaji Wakiaga alisema Katitu alikosa kufuata sheria za kulinda maisha ya binadamu alipomuua Kimani na nduguye Oscar Mwangi Machi 2013.

“Lazima kila afisa wa polisi ajue jukumu lake la kwanza ni kulinda maisha ya kila mmoja wahalifu wakiwamo,” alisema Jaji Wakiaga akiongeza, “Polisi wanatakiwa kisheria kutumia kila mbinu kumtia nguvuni mshukiwa aadhibiwe kisheria badala ya kutamatisha maisha yake.”

Mahakama ilisema ijapokuwa Katitu alikuwa anashambikiwa mno na wakazi wa Githurai walioomba korti imwachilie mshtakiwa arudi kuwatumikia kwa vile "aliwapiga risasi majambazi hadi uhalifu ukapungua kwa kiwango kikubwa hapa”.

Sheria

Jaji Wakiaga alisema ingawa msimamo wa wakazi wa Githurai ni 'mzuri', sheria inasema mengine.

“Sheria inawataka maafisa wa polisi wazingatie sheria hata wakiwa na umaarufu wa kupambana na wezi. Polisi hawapaswi kuwatoa uhai washukiwa mbali wanatakiwa kutumia kila mbinu kuwashika na kuwafikisha kortini kuadhibiwa kisheria.”

Mahakama ilisema mshtakiwa alimpiga Kimani risasi mara tatu kichwani na kumuua kabisa.

“Sifa za kuogopwa kwa Katitu zilienea kote jijini Nairobi na maeneo jirani na hata wahalifu walimtambua. Angetumia sifa hizo kuwatisha wahalifu kwa kupiga risasi angani ama kutumia mbinu nyingine kuwashika badala ya kuwaua,” alisema Jaji Wakiaga.

Jaji huyo alisema sheria nambari 204 ambayo washukiwa wa mauaji huhukumiwa inatoa adhabu moja tu - ya kifo.
Hata hivyo alisema kulingana na uamuzi wa Mahakama ya Juu wa hivi majuzi majaji wanatakiwa kutilia maanani malilio ya mshtakiwa kabla ya kupitisha hukumu.

Jaji Wakiaga alisema ijapokuwa kumekuwa na kampeni ya vyombo vya habari mshtakiwa aachiliwe, sheria inasema mengine.

Alisababisha kicheko aliposema upeperushaji wa baadhi ya maoni ndio unafanya Waziri wa Usalama Fred Matiang’i atukane majaji wa mahakamani baada ya baadhi ya vituo vya habari kuwanukuu baadhi ya watazamaji wakitoa wito Katitu aachiliwe wakisema “wahanga walikuwa wahalifu”.

Jaji huyo alisema Katitu alivunja sheria kuwaua Kimani na Oscar na kuamuru afungwe jela.

AFISA WA POLISI AHUKUMI WA MIAKA 15 JELA KWA KUFANYA MAUAJI AFISA WA POLISI AHUKUMI WA MIAKA 15 JELA KWA KUFANYA MAUAJI Reviewed by KUSAGANEWS on April 05, 2018 Rating: 5

No comments: