SERIKALI YA KENYA YAANZA KUTEKELEZA MKAKATI KUPUNGUZA MSONGAMANO THIKA SUPERHIGHWAY


WAZIRI wa Uchukuzi James Macharia amesema kuwa nauli zinazotozwa hasa na matatu Jijini Nairobi lazima zipungue kufuatia juhudi mpya za kutenga barabara zitakatotumika na magari hayo pekee.

Waziri ambaye alikuwa mbele ya Kamati ya Seneti ya Barabara alisema kuwa wanaanza majaribio ya mpango huo na barabara ya Thika Superhighway, ambapo kutakuwa na barabara iliyotengewa magari ya uchukuzi wa umma kutoka mtaa wa Githurai hadi katikati mwa jiji.

“Nauli zinastahili kupungua, lazima zipungue. Wachukuzi wa magari ya umma wamekuwa wakisema kuwa nauli ziko juu kwa sababu ya muda mwingi wanaokaa kwa msongamano barabarani. Tunaanza na njia ya moja kwa moja kutoka Githurai hadi Katikati mwa Jiji katika barabara ya Thika.

Nauli inayotarajiwa kulipwa ni Sh40,” amesema Dkt Macharia.

Waziri ameeleza kuwa mbali na mabasi ya Huduma ya Vijana kwa Taifa (NYS), Wamiliki wa Matatu pia wanatarajiwa kuleta nchini mabasi 50 ambayo yatatumika kuimarisha usafiri jijini.
Wamiliki wa matatu wamepinga mpango wa serikali kuingilia biashara hiyo wakihofia kuwa inalenga kuwasambaratisha.
Nauli

Macharia aliambia kamati hiyo inayoongozwa na Seneta wa Kiambu, Bw Kimani Wamatangi, kuwa ingawaje nauli humu nchini hazijadhibitiwa, mpango huo wa kutenga barabara utasaidia katika kushauri kiasi cha nauli kinachofaa.

Wakati huo huo, waziri alieleza kuwa huduma hiyo inatoa suluhisho la muda, kwa uchukuzi na sekta hiyo inawahitaji wawekezaji wa kibinafsi kuhusika.
Pia alisema wanatarajia kuwa matatu za abiria 14 zitaondolewa kabisa barabarani katika harakati za kuboresha uchukuzi jijini.

Jiji la Nairobi aliambia kamati hiyo linahitaji takriban mabasi 900 kuweza kuendesha vilivyo usafiri unaotegemewa, na ambao utakuwa na viwango vinavyowavutia Wakenya wa ngazi zote.


SERIKALI YA KENYA YAANZA KUTEKELEZA MKAKATI KUPUNGUZA MSONGAMANO THIKA SUPERHIGHWAY SERIKALI YA KENYA YAANZA KUTEKELEZA MKAKATI KUPUNGUZA MSONGAMANO THIKA SUPERHIGHWAY Reviewed by KUSAGANEWS on April 05, 2018 Rating: 5

No comments: