UJUMBE WA MAMA SAMIA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI


Makamu Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka wananchi kwa pamoja kuunga mkono jitihada zinazofanywa na serikali ya awamu ya tano ili waweze kuifikisha nchi katika uchumi wa kati.

Mama Samia ametoa kauli hiyo wakati alipokuwa akitoa salamu zake katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani leo Machi 8, 2018 ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema kuelekea uchumi wa viwanda tuimarishe usawa wa kijinsia na uwezeshaji wa wanawake vijijini.

"Tuimalishe sasa maendeleo ya wanawake kushuka kule vijijini, tuwaibue wa vijijini na wenyewe waweze kujua ni jambo gani linaendelea ili watoe mchango wao katika kuelekea Tanzania ya viwanda.  Katika kuandimisha siku hii ya wanawake duniani, ninawaombe kwa dhati kabisa muunge mkono serikali katika jitihada zote ambazo tunafanya", amesema Mama Samia. 

Pamoja na hayo, Mama Samia ameendelea kwa kusema "kila mmoja pale alipo aunge mkono serikali ili azma tuliyoikusudia iweze kutimia na sote kwa pamoja tuingie kwenye maendeleo ya viwanda na tuipeleke nchi yetu kwenye uchumi wa kati pale itakapofika 2025".

Kwa upande mwingine, Makamu wa Rais amesema mpaka sasa jitihada serikali ya Tanzania imefanya katika kuhakikisha inamuinua mwanamke na itaendelea kufanya hivyo siku zote.

UJUMBE WA MAMA SAMIA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI UJUMBE WA MAMA SAMIA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI Reviewed by KUSAGANEWS on March 08, 2018 Rating: 5

No comments: