UCHUMI WA RWANDA WAKUA KWA ASILIMIA 6.5 KUTOKA ASILIMIA 4.9


Benki kuu ya Rwanda imesema uchumi wa nchi hiyo unakadiriwa kukua kwa asilimia 6.5 kwa mwaka huu.

Gavana wa benki ya Rwanda Bw John Rwangombwa amesema kiwango cha mfumko wa bei kwa mwaka huu kinakadiriwa kuongezeka hadi asilimia 5 ikilinganishwa na asilimia 4.9 ya mwaka jana.

Pia amsema mwaka jana mapato yaliyotokana na uuzaji wa bidhaa nje yaliongezeka kwa asilimia 57.6, na uagizaji wa bidhaa kutoka nje ulipungua kwa asilimia 0.4 ikilinganishwa na mwaka 2016. 

Zaidi ya hayo, aina za bidhaa zilizouzwa nje zinaendelea kuongezeka.
Takwimu zilizotolewa na benki hiyo zinaonyesha kuwa mwaka jana urari wa biashara ulipungua kwa asilimia 21.7 ikiliganishwa na mwaka 2016.

UCHUMI WA RWANDA WAKUA KWA ASILIMIA 6.5 KUTOKA ASILIMIA 4.9 UCHUMI WA RWANDA WAKUA KWA ASILIMIA 6.5 KUTOKA ASILIMIA 4.9 Reviewed by KUSAGANEWS on March 07, 2018 Rating: 5

No comments: