Bodi ya ligi kuu (TPLB)
imepangua ratiba ya ligi kuu soka Tanzania bara kwa mchezo mmoja kati ya Mbao
FC dhidi ya Lipuli FC, uliokuwa umepangwa kuchezwa April 9 kwenye uwanja wa CCM
Kirumba.
Mchezo huo namba 184 wa ligi, sasa
umerudisha nyuma hadi April 6 na utachezwa kwenye uwanja huo huo wa CCM Kirumba
jijini Mwanza.
Sababu za mchezo huo kurudishwa
nyuma zimeelezwa kuwa ni kuipa nafasi timu ya Mbao FC kupumzika na kujiandaa na
mchezo wa ligi kuu dhidi ya Njombe Mji utakaopigwa April 11 CCM Kirumba.
Afisa mtendaji mkuu wa Bodi ya Ligi
Boniface Wambura, tayari ameshatuma taarifa kwa klabu hizo na kuzitaka
kuzingatia mabadiliko hayo ili kuepuka usumbufu unaoweza kujitokeza.
Ratiba ya VPL yabadilika
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 07, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 07, 2018
Rating:



No comments:
Post a Comment