Raisi wa TFF Wellace Karia asikitishwa kifo cha Rais


Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Wallace Karia ametuma salamu za pole kwa Chama cha Mpira wa Miguu Cyprus kufuatia kufariki kwa aliyekuwa Rais wa FA Costakis Koutsokoumnis akiwa na umri wa miaka 61.

Karia ametoa salamu hizo baada ya kupokea taarifa ya kifo kilichotokea Machi 5, 2018 na kusema amesikitushwa kwa kiasi kikubwa kwa kumpoteza mmoja wa viongozi wakongwe wa mpira wa miguu.

"Koutsokoumnis alikuwa muhimiri mkubwa kwa soka la Cyprus na amefariki katika wakati ambao Cyprus na mpira kiujumla ulikuwa una muhitaji, nimesikitishwa na kifo chake na ninatoa pole kwa familia yake, FA ya  Cyprus, FIFA pamoja na familia ya soka kwa ujumla", amesema Rais Karia.

Mpaka mauti yanamkuta Koutsokoumnis alikuwa ndio Rais wa FA ya Cyprus na amekuwa kwenye kamati mbalimbali za FIFA akiwa Makamu Mwenyekiti na alianza kutumikia soka la Cyprus tokea mwaka 1990. Amewahi kuwa Makamu wa Rais wa FA ya Cyprus kabla ya kuchaguliwa kuwa Rais wa FA  mwaka 2001 nafasi aliyoitumikia mpaka mauti yanamkuta.

Raisi wa TFF Wellace Karia asikitishwa kifo cha Rais Raisi wa TFF Wellace Karia asikitishwa kifo cha Rais Reviewed by KUSAGANEWS on March 07, 2018 Rating: 5

No comments: