Man United na Crystal Palace zaacha rekodi hizi


Baada ya klabu ya Manchester United kutokea nyuma na kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 jana usiku dhidi ya Crystal Palace, mechi hiyo imeacha rekodi mbalimbali katika ligi kuu ya England.

Moja ya rekodi ni klabu ya Manchester United kutokea nyuma kwa  mabao 2-0, na kushinda mchezo wa Ligi Kuu kwa mara ya kwanza tangu ifanye hivyo Desemba 2013 ugenini dhidi ya Crystal Palace.

Kwa upande wa Crystal Palace jana ndio ilikuwa mechi yao ya kwanza kupoteza baada ya kuwa wanaongoza kwa mabao 2-0 au zaidi. Pia Crystal Palace hawajashinda mechi 20 sasa dhidi ya United ikiwa ni idadi kubwa ya mechi kuliko timu zote walizokutana nazo.

Rekodi nyingine ni bao la kwanza la Nemanje Matic kwa tangu ajiunge na United huku likiwa ni bao la ushindi la dakika ya 90  kwa United tangu alipofunga bao la ushindi Marcus Rashford dakika ya 90 dhidi ya Hull City mwaka 2016.


Man United na Crystal Palace zaacha rekodi hizi Man United na Crystal Palace zaacha rekodi hizi Reviewed by KUSAGANEWS on March 06, 2018 Rating: 5

No comments: