Upelelezi wa kesi inayomkabili Mhasibu Mkuuwa TAKUKURU, Godfrey Gugai ya
kumiliki mali za Shilingi Bilioni 3 zisizoendana na kipato chake haujakamilika
katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu ikiwa ni siku 110 tangu afikishwe
mahakamani hapo.
Gugai alifikishwa
mahakamani hapo kwa mara ya kwanza November 16,2017.
Wakili wa serikali Mwandamizi, Mutalemwa Kishenyi amemueleza
Hakimu Mkazi Mkuu, Thomas Simba kuwa
upelelezi wa shauri hilo bado haujakamilika.
Pia ameeleza kuwa jalada la
kesi hiyo bado lipo kwa Mkurugenzi wa Mashtaka (DPP) kwa ajili ya kulipitia na
kulitolea maamuzi.
Baada ya kueleza hayo Hakimu Simba aliutaka upande wa mashtaka kuhakikisha
upelelezi unakamilika ambapo ameahirisha kesi hiyo hadi March 20,2018.
Mbali na Gugai, washtakiwa
wengine katika kesi hiyo ni George Makaranga, Leonard Aloys na Yasini Katera.
Washtakiwa hao wanaokabiliwa na
mashtaka 43 yakiwemo 20 ya utakatishaji fedha haramu, kumiliki mali
zisizoendana na kipato na kughushi mikataba ya mauziano ya viwanja katika
maeneo mbalimbali.
Kesi ya mtuhumiwa anaemiliki mali zisizoendana na Kipato yakwama
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 06, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 06, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment