BENKI YA WANAWAKE TWB YADAI MIKOPO SUGU YENYE THAMANI YA SH BILIONI 7,6 TOKA KWA WATEJA ZAIDI YA 7000
Benki ya Wanawake Tanzania (TWB) katika hatua zake za kutaka kuimarisha mtaji wake na kufanya kazi zake kwa ufanisi imewataka wateja wake 7,065 wenye mikopo sugu yenye thamani Tsh. bilioni 7.9, kulipa mikopo hiyo ndani ya siku saba vinginevyo watachukuliwa hatua za kisheria.
Akizungumza na
waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa bodi ya
benki hiyo, Bi. Ben Issa alisema benki imeanza kuchukua hatua za kuimarisha
mtaji wake kwa kuwataka wateja wake wenye madeni sugu kulipa madeni yao ndani
ya siku hizo vinginevyo hatua za kisheria zitachukuliwa.
Moja ya mambo
yanayokwamisha kuimarika kwa mtaji na
kupanua huduma za kibenki ni kuwepo kwa mikopo sugu sasa tunawataka wateja wetu
wenye mikopo sugu kulipa bila shuruti vinginevyo hatua za kisheria
zitachukuliwa, aliongeza kusema,Bi Issa ambaye pia ni Katibu Mtendaji wa Baraza
la Taifa la Uwezeshaji Wananchi Kiuchumi (NEEC
Alisema hatua
hiyo imechukuliwa ili kuhakikisha mtaji wa benki unaimrika na itasaidia kutoa
huduma za kibenki kwa ufanisi. Wakopaji wengi wamepitiliza siku 90 za
urejeshaji madeni ya mikopo yao na hiyo kinyume na utaratibu wa mikataba
waliyokubaliana na benki wakati wanakopa.
BENKI YA WANAWAKE TWB YADAI MIKOPO SUGU YENYE THAMANI YA SH BILIONI 7,6 TOKA KWA WATEJA ZAIDI YA 7000
Reviewed by KUSAGANEWS
on
March 07, 2018
Rating:

No comments:
Post a Comment