|
MKUU wa
Wilaya ya Longido, Daniel Chongolo, amesema wanatarajia kuanza ukaguzi wa
boma kwa boma kuwabaini watoto waliokeketwa na kuwachukulia hatua
za kisheria wazazi
|
|
Alisema
hayo katika uzinduzi wa kampeni ya kupinga mimba na ndoa za utotoni kwa
ngazi ya wilaya iliyoandaliwa na Mratibu wa Miradi wa Kitumbeine, ulio
chini ya Shirika la World Vision Tanzania (WVT
Mradi
huo unajihusisha na masuala ya afya, elimu, utetezi, kilimo, mifugo na
uchumi.
|
|
Hata
hivyo, alisema, hawezi kutaja siku ya kuanza ukaguzi huo utakaowashirikisha
maafisa afya kwa kila boma.Alisema ukaguzi huo utahusisha pia watu
waliowapa mimba watoto na kuwaoa
|
|
“Wapo
wanaooa mimba, baadaye wanajipitisha kwa kutengeneza mazingira ya kuwapa
mimba, hakutakuwa na mswalia Mtume kwa jambo hili,”
alisema.
|
|
“Nitaanza
na hilo, wataalam wa afya watapita kufanya ukaguzi wa watoto, wakibainika
wazazi wao watafikishwa mahakamani,” alisema
|
|
Alisema
uamuzi wa kufanya ukaguzi umekuja baada ya kubaini kwamba hakuna watu
wanaofikishwa kwenye vyombo vya sheria kwa kufanya ukatili huo.
|
|
|
|
No comments:
Post a Comment