Kiongozi wa chama cha
Act Wazalendo Taifa Zitto Kabwe, amewataka wanachama wa ACT Wazalendo
kutotereka na hali ya siasa ambayo kuna ubinywaji wa demokrasia na kusisitiza
kuwa nchi hii haiwezi kurudi kwenye mfumo wa chama kimoja licha ya nguvu nyingi
kutumika ya kuua upinzani.
Alisema kinachopaswa
kufanyika ni kusimama imara na kupigania demokrasia ya kweli ambayo itawafanya
watu kuwa huru na kufanya kile wanachokitaka bila ya kuvunja sheria za nchi.
Zitto ameyasema hayo
leo Februari 28 mjini Shinyanga akiwa kwenye ziara yake ya kuimarisha chama
alipokutana kuzungumza na viongozi pamoja na wanachama wa chama hicho mjini
humo, na kuwataka wasitetereke na uendeshwaji wa siasa hapa nchini na kuanza
kuhama vyama hovyo bali wajipange kisaikolojia na kukijenga chama.
Alisema siasa za sasa nchini Tanzania ni ngumu, hivyo wasikate tamaa kuendeleza mapambano ya kupigania demokrasia hapa nchini, pamoja na kuendelea kuulinda mfumo wa vyama vingi ambao ndiyo mkombozi kwa watanzania na waendelee kujipanga kugombea majimbo katika chaguzi hizo ukiwemo uchaguzo mkuu wa mwaka 2020.
Zitto Kabwe alieleza
kuwa kutokana na jambo hilo la kubinywa kwa demokrasia hapa nchini wanapaswa
kujiandaa kisaikolojia kwenye chaguzi hizo na kutotishika na watu wanaohama
vyama vya siasa, bali waanze kujipanga mapema namna ya kulinda wizi wa kura,
kutafuta mawakala waaminifu pamoja na viongozi kutatua kero za wananchi.
“Tunataka chama chetu
kiwe tofauti na vyama vingine vya upinzani kwa kutohama hama vyama kwa kuhofia
uchaguzi mkuu ujao kuwa hawatopata kura wala uongozi, bali sisi tujipange
kisaikolojia na kufanya kazi ya kusikiliza na kutatua kero za wananchi, ambao ndio
wenye ridhaa ya kutupatia uongozi,”alisema.
Aliwataka viongozi wa
chama hicho ambao walipewa ridhaa ya wananchi kwenye chaguzi zilizopita
(2014-15) za serikali za mita,madiwani na ubunge wawatumikie wananchi ipasavyo
kwa kutatua kero zao ili kuonyesha utofauti wa viongozi wa ACT na wa vyama
vingine ili kuendelea kukiimarisha chama kwa wananchi.
Nao baadhi ya
wanachama hao akiwemo Maarufu Hassani, walionyesha wasiwasi juu ya baadhi ya
viongozi ambao walipata ridhaa kwenye chaguzi zilizopita (2014-15) kuwa
kutokana na vuguvugu la kisiasa hapa nchini la kubinywa kwa demokrasia na
chaguzi zinavyoendeshwa kuwa kuna uwezekano wa viongozi hao wasirudi 2020.
Katika ziara hiyo,
Zitto alifanikiwa kuvuna wanachama wapya Tisa kutoka vyama mbalimbali vya siasa
ambapo aliwapatia kiapo cha utii wa chama hicho ili kuendelea kukilinda na
kukijenga chama kwa wananchi ambao ndio watawapatia ridhaa ya kushika nchi.
ZITO NCHI HAIWEZI KURUDI KWENYE MFUMO WA CHAMA KMOJA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment