Klabu ya soka ya Azam FC kupitia kwa kocha wake msaidizi Idd Cheche imesema itaingia kwa tahadhari kwenye mchezo wao wa raudni ya 20 ligi kuu soka Tanzania bara dhidi ya Singida United.
“Tahadhari lazima tuingie nayo iwe
nafasi yoyote uliyokuwepo lakini lazima tuingie na tahadhari kwa sababu
hatutaki kufungwa tunataka kushinda kwanza'', amesema.
Cheche amesisitiza kuwa wataweka
usalama katika ulinzi ili kuhakikisha mpira hauingii kwenye nyavu zao halafu
watengeneze mipango ya kuhakikisha wanapata magoli ambayo yatawapa ushindi ili
wazidi kuwakimbia Singida United.
Azam FC ipo katika nafasi ya tatu
kwenye msimamo wa ligi ikiwa na pointi 35, huku Singida United ikiwa nafasi ya
nne na alama 34 na zitakutana Jumamosi hii kwenye uwanja wa Azam Complex.
Katika mchezo wa raundi ya kwanza
timu hizo zilipokutana zilitoka sare ya 1-1 katika mchezo uliopigwa kwenye
uwanja wa Jamhuri Morogoro. Singida United ilikuwa inatumia uwanja huo kabla ya
kurudi Namfua mjini Singida.
AZAM WACHUKUA TAHADHARI KABLA YA HATARI
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 28, 2018
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
February 28, 2018
Rating:


No comments:
Post a Comment