Aliyekuwa kaimu kamishna wa madini asomewa maelezo ya awali



Kesi ya matumizi mabaya ya madaraka inayomkabili aliyekuwa Kaimu Kamishna wa Madini kutoka Wizara ya Nishati na Madini, Ally Samaje, imeshindwa kuendelea baada ya upande wa mashtaka kudai kuwa hawajaanda maelezo ya awali.

Kwa mara ya kwanza, Samaje alifikishwa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, Februari 9, 2018 kujibu mashtaka mawili ya matumizi mabaya ya madaraka.

Wakili kutoka Takukuru, Leonard Swai amedai leo Februari 28, 2018 mbele ya Hakimu Mfawidhi, Victoria Nongwa, kuwa kesi hiyo ilikuja kwa ajili ya mshtakiwa kusomewa maelezo ya awali, lakini bado hawajaanda

“Shauri hili lilikuja kwa ajili ya mshtakiwa kusomewa hoja za awali, lakini bado hatujaziandaa, hivyo tunaomba tarehe nyingine kwa ajili ya kuziandaa na kumsomea” alidai Swai

Baada ya maelezo hayo, hakimu Nongwa ameahirisha kesi hiyo hadi Machi 28, 2018 itakapokuja kwa ajili ya kusomewa maelezo ya awali na mshtakiwa yupo nje kwa dhamana.

Katika kesi ya msingi, Swai amedai kuwa mshtakiwa huyo alitenda makosa hayo kati ya Aprili 9 na Juni 21, 2013 Makao Makuu ya Wizara ya Nishati na Madini iliyopo wilaya ya Ilala.

Hata hivyo, Samaje ambaye anatetewa na wakili Jema Bilegea, yupo nje kwa dhamana baada ya kusaini ahadi ya Sh 50milioni na hatakiwi kusafiri nje ya nchi bila kibali cha mahakama.

Aliyekuwa kaimu kamishna wa madini asomewa maelezo ya awali Aliyekuwa kaimu kamishna wa madini asomewa maelezo ya awali Reviewed by KUSAGANEWS on February 28, 2018 Rating: 5

No comments: