Jumla ya watu 77 walipoteza maisha katika mkoa wa Kagera
kutokana na matukio ya ajali za barabarani 79 zilizotokea mkoani humo katika
kipindi cha kuanzia mwezi januari hadi Septemba mwaka huu zilizosababishwa na
waendesha magari na pikipiki.
Hayo yameelezwa na mrakibu mwandamizi wa jeshi la polisi,
William Mkonda ambaye mkuu wa kikosi cha usalama barabarani mkoani Kagera wakati
wa kufunga wiki ya nenda kwa usalama wilayani ngara iliyoandaliwa na mkoa wa
Kagera kuanzia Septemba 26, mwaka huu,
Akizungumza wakati akielezea mambo
yanayosababisha ajali katika mkoa huo, amesema kwa sasa ajali zimepungua kwa
kuwa mwaka jana katika kipindi cha kuanzia mwezi januari hadi Septemba jumla ya
watu 81 walipoteza maisha kutokana na ajali 102 za magari na pikipiki.
Kwa upande wake, mwenyekiti wa kamati ya usalama barabarani
ya mkoa wa Kagera, Winston Kabanteba ameeelezea shughuli mbalimbali
zilizofanyika katika wiki ya nenda kwa usalama, akizungumza amesema katika wiki
hiyo
Elimu ya masuala ya usalama barabarani imetolewa kwa waendesha pikipiki na
wanafunzi ambao wanasoma kwenye shule zilizoko kando ya barabara, naye mkuu wa
wilaya ya ngara,Luteni Kanali Michael Mntenjele amewataka waendesha vyombo vya
moto kwa kuzingatia kauli mbiu ya jeshi la polisi ya kutii sheria bila shuruti.
WATU 77 WAPOTEZA MAISHA KUTOKANA NA AJALI ZA BARABARANI KUANZIA SEPTEMBA 26 MWAKA HUU MKOANI KAGERA
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 09, 2016
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 09, 2016
Rating:


No comments:
Post a Comment