MADIWANI wanne akiwemo mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha wafikishwa mahakama ya mwanzo Enaboishu Wilayani Arumeru.
Mahakama ya mwanzo ya Enaboishu iliyopo Wilayani Arumeru Mkoani
Arusha Jana imewasomea mashtaka madiwani wanne akiwamo mwenyekiti wa
Halmashauri ya Arusha Noah Lembris.
Aidha katika mashtaka yaliyosomwa mbele ya Hakimu David Dhahabu
yalieliza kuwa viongozi hao wakabiliwa na shtaka la kutoa lugha ya kashfa kwa
mkuu wa Wilaya ya Arumeru Alexander Mnyeti.
Askari aliyesoma mashtaka hayo alisema madiwani hao walitoa
lugha za kashfa kuwa "mkuu wa Wilaya siyo polisi,nyingine Serikali
ina ubabe katika kutekeleza majukumu ya CCM.
Kashfa nyingine "mkuu wa Wilaya anatumia masaa masaa
48 kuwaweka viongozi ndani ambapo wahishtakiwa walikana mashtaka hayo
kuwa si ya kweli.
Hata hivyo mashtaka hayo yanaeleza kuwa kutoa lugha za kashfa
kwa viongozi ni kinyume cha sheria kwa mujibu wa kifungu cha sheria cha
89 kifungu kidogo cha 16 kanuni ya adhabu ambapo ilifanyiwa marekebisho 2002.
Baada ya hakimu Dhahabu kusikiliza mashtaka hayo alimtaka askari
huyo aliyesoma mashtaka hayo kumwandikia barua ya kumtaka mlalamikaji
kufika mahakamani siku ya kusikilizwa kwa kesi hiyo.
Kesi hiyo inatarajiwa kusikilizwa mapema oktoba 24 majira
ya saa 3:00 ambapo washtakiwa wapo nje kwa dhamana ya laki 5
kwa kila mmoja na wadhamini wawili.
Waliofikishwa mahakamani hapo ni pamoja na Mwenyekiti wa
Halmashauri ya Arusha Noah Lembris, Happy Gadiel Diwani Viti maalum, Winfrida Lukumay na Nuru Ndosi.
Halmashauri ya Arusha Noah Lembris, Happy Gadiel Diwani Viti maalum, Winfrida Lukumay na Nuru Ndosi.
Wakiongea nje ya mahakama hiyo viongozi hao walisema
ni uonevu na ukandamizaji wa haki za binadamu walichofanyiwa.
Mwenyekiti Lembrisi alisema mkuu wa Wilaya ameamua
kuwadhalilisha Chadema ambapo alisema nikudhohofisha chama.
"Pamoja na kutaka kutudhohofisha
Chama sisi hatutarudi nyuma maana tunaamini hawezi kufanikiwa kutudhohofisha kwa sheria zake kandamizi anazozileta"
alisema Lembrisi.
Chama sisi hatutarudi nyuma maana tunaamini hawezi kufanikiwa kutudhohofisha kwa sheria zake kandamizi anazozileta"
alisema Lembrisi.
Alisema wanasikitika kusikia mkuu huyo anajiita rais wa
Arumeru wakati nchi hii inaongozwa na rais mmoja tu ambaye ni John Magufuli.
" Nia ya Dc ni kuvuruga juhudi za
maendeleo zinazofanywa na viongozi wa Chadema ila tunamwambia sisi
anapotuweka mbali ndivyo anavyozidi kutufanya tuwe ngangari kwa kupambana zaidi
kuwaletea wananchi maendeleo " alisema .
Aliongeza kuwa hadi sasa wenyeviti zaidi ya saba wa maeneo
mbalimbali ya Arumeru wapo ndani kwa masaa 48 kutokana na amri ya mkuu huyo wa
Wilaya.
Naye mwanasheria wa Chadema Charles Abraham alisema anashangazwa
na vitendo vya Dc vya kuingilia kazi za madiwani kwani siyo sheria kuomba
ruhusa kufanya shughuli za maendeleo kwa wananchi wao.
" Rai yangu kwa rais ni kwamba anapoteua viongozi wa
kuongoza Wilaya aangalie vigezo zaidi watu wasiojua sheria hawawezi
kuongoza watu" alisema.
Alisema hakuna sheria iliyooanishwa katika kesi iliyopelekwa
mahakamani inayowatuhumu viongozi hao hivyo ni kesi ambayo haieleweki.
"Sisi kama chama tunalaani vikali vitendo anavyovifanya
kiongozi huyu na sidhani kama anafaham sheria kuna maslahi yoyote mapana
ya taifa yaliyoingiliwa ili apate kuwatuhumu vizuri " alihoji.
" Hata kama anaisoma sheria huenda haielewi maana
haiwezekani kama viongozi wana tekeleza majukumu ya kimaendeleo
yeye atoe amri wakamatwe badala ya kuungana nao kuleta maendeleo" alisema
mwanasheria huyo.
Alisema wao kama chama wanachukua hatua za kisheria kuomba kesi
ihamishiwe mahakama ya Wilaya ili ipate kusimamiwa na mawakili.
Kwa upande wake Diwani Viti maalum ambaye ni mshtakiwa Happy
Gadiel alisema ni nguvu nyingine wanayo ongezewa kwa kuwekwa ndani kutokana na
kuwatumikia wananchi waliowachagua.
"Ninawaambia tu wananchi wangu kuwa sitakata tamaa kutafuta
maendeleo kwa sababu ya aina yoyote ile sisi tumejipanga na maendeleo yatakuja
tu" alisema Gadiel.
Wakati huohuo Mwenyekiti wa kijiji cha Kimyaki kilichopo
Wilayani hapo alifikishwa Mahakaman kwa kosa hilo hilo la kutoa lugha zakashfa
kwa mkuu huyo wa Wilaya.
Mwenyekiti huyo jina Alphayo Michael alisomewa mashtaka ya
kutoa kashfa kwa Dc katika mkutano wake na wana kijiji
uliofanyika agost 8 mwaka huu.
Jambo hilo limewashangaza waliohudhuria Mahakamani kutokana na
mashtaka kufanana huku viongozi hao wakiwa wanatokea maeneo tofauti.
MADIWANI wanne akiwemo mwenyekiti wa Halmashauri ya Arusha wafikishwa mahakama ya mwanzo Enaboishu Wilayani Arumeru.
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 17, 2016
Rating:
Reviewed by KUSAGANEWS
on
October 17, 2016
Rating:


No comments:
Post a Comment