WADAU WA UTALII KUKUTANA KESHO ARUSHA 22 SEPTEMBA KWENYE UKUMBI WA AICC





Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika mkutano wa siku moja wa wadau wa sekta ya Utalii mkoani Arusha unaotarajiwa kufanyika kesho.

Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo amesema kuwa mkutano kama huo utakaofanyika kesho ulifanyika kwa mara ya mwisho mwaka 2012 hivyo wameona ni vema serikali kushirikiana na wadau wa utalii kukaa pamoja kujadili changamoto mbalimbali zinazowakabili  ili kuboresha sekta hiyo.
Amesema kuwa mkoa wa Arusha ni kitovu cha cha utalii na unachangia pato la mkoa kwa asilimia 20% na kitaifa kwa asilimia 17%ambapo mwaka 2015 idadi ya watalii iliyoingia nchini ilikuwa 1,137,182 na kuingizia Taifa kiasi cha dola za kimarekani milioni 1.9 na kwamba katika idadi hiyo asilimia 80%watalii walitembelea mkoa  kwasababu ya vivutio vingi vilivyopo mkoani humo.

Vilevile Gambo amesema kuwa katika mkutano huo wadau mbalimbali watapata fursa ya kumuliza maswali waziri mwenye dhamana kwa upande wa utalii ili kuondoa baadhi sintofahamu kwa baadhi ya maeneo kuhusu sekta ya utalii kwa upande wa utalii.

”Wale wadau mbalimbali ambao watahitaji kuwa na maswali pengine ya kupata majibu ya moja kwa moja kutoka kwa mhesahimiwa waziri atakuwepo na amejidhatiti kutoa maelekezo vizuri ili kuondoa sintofahamu””

Pamoja na hayo ameongeza kuwa tarehe 27 septemba ni siku ya kusherekea siku ya utalii duniani ambapo kauli mbiu ya mwaka huu inasema UTALII KWA WOTE  na kwa mkoa wa arusha wameanza mapema ili kujadili masuala mbalimbali ili ifikapo tarehe rasmi iwe ni siku ya kutoa muelekeo wa hali ya utalii katika mkoa wa arusha na tanzania kwa ujumla.
WADAU WA UTALII KUKUTANA KESHO ARUSHA 22 SEPTEMBA KWENYE UKUMBI WA AICC WADAU WA UTALII KUKUTANA KESHO ARUSHA 22 SEPTEMBA KWENYE UKUMBI WA AICC Reviewed by KUSAGANEWS on September 21, 2016 Rating: 5

No comments: