WATUMISHI WA SERIKALI ARUSHA MSIWE KAMA MIUNGU WATU TATUENI KERO ZA WANANCHI



Mkuu wa wilaya ya arusha Mjini Bwana Gabriel Fabian Daqaro

Mkuu wa wilaya ya Arusha mjini Gabriel  Fabian  Daqaro amewataka watumishi wa serikali kuhakikisha wanafanya kazi kwa bidii ili kutatua kero za wananchi zinazowasumbua katika maeneo yao kwenye maeneo yao.

Daqaro amesema hayo wakati akizungumza na watumishi wa serikali katika halmashauri ya jiji la arusha na kusema kuwa kuna baadhi ya watumishi wa serikali wamekuwa wakijifanya kama Mungu watu kwa kutoa maneno ya kashfa kwa wananchi pamoja kushindwa kutatua kero zinazowakumba wananchi.

Pia mewataka watumishi wa serikali kuwatendea haki wananchi
Wanapohitaji huduma pidi wanapofika katika ofisi zao na wasiwanyanyase kwa wananchi ndiyo wateja namba moja na ndiyo wamemchagua raisi wa jamhuri ya muungano wa Tanzania John Pombe magufuli.

Kwa upande wake Mkurugenz wa jiji la arusha Athumani kihamia amesema kuwa watumishi wanalipwa mshahara kila mwezi hivyo hawezi mvumilia mtendaji yeyote katika kitengo chochote cha halmashauri anaenda kinyume na taratibu na kushindwa kuhudumia wananchi na kutatua kero zao.
Mkurugenzi wa jiji la Arusha Athumani Juma kihamia akiwa ameshika kipaza sauti 
Pamoja na hayo Kihamia amesema kuwa kuna baadhi ya watumishi wa serikali wanawanyanyasa wananchi na wakati mwingine mpaka waandishi wa habari ambao wanawasaidia kutoa taarifa ambazo jamii inatakiwa izitambue jambo ambalo amesema hatovumilia watumishi wenye tabia hizo za unyanyasaji.
WATUMISHI WA SERIKALI ARUSHA MSIWE KAMA MIUNGU WATU TATUENI KERO ZA WANANCHI WATUMISHI WA SERIKALI ARUSHA MSIWE KAMA MIUNGU WATU TATUENI KERO ZA WANANCHI Reviewed by KUSAGANEWS on September 17, 2016 Rating: 5

No comments: