HAKUNA ATAKAEFUNGUA OFISI ASEMA MWENYEKITI UVCCM ARUSHA




Ofisi ya UVCCM  mkoa wa Arusha yapigwa mnyororo mwenyekiti wa umoja huo Ole Sabaya asema  waliofunga ni vibaka avunja kofuli na kufungua ofisi hiyo.

Akizungumza  nje ya ofisi hiyo Mwenyekiti Wa Uvccm mkoa Martin  Ole Sabaya  amesema waliofunga ofisi ni vibaka na hawatambui hivyo alisema ofisi yake haiwezi kuingiliwa ovyo.

" Hawa waliofunga ofisi ni vibaka tena waizi  wakubwa hatujakaa tukatafakari mali zilizopotea ndani ya ofisi ili kubaini  na wachache waliofanya hivi tumeshawajua" alisema Ole Sabaya.

Alisema hakuna Katibu anateruhusiwa kuingia hapo aliyeripoti na aliyekuwepo hakuna anayeruhusiwa bali  hadi  baraza litakapo kaa  ndipo maamuzi yatakapo tolewa.

Mwenyekiti huyo alisema wapo watu  ambao ni wanachama lakini wanakihujumu chama hivyo hawezi kukubaliana na hilo.

Alisema wasiompenda waombe Mungu awahi kumaliza uongozi wake mapema kwani yeye hawezi kuhamishwa kama  makatibu hivyo atapambana kuhakikisha maslahi ya chama yanaonekana.

Ofisi hiyo ilifungwa alfajiri Jana majira ya saa  10  ambapo walikuja kikundi cha watu wakaanza kupambana na askari waliokuwa  wakilinda eneo hilo kwa kuwatupia mawe  na hatimaye wakafanikiwa kuweka kofuli yao.

Baada ya muda alifika mwenyekiti huyo na kuvunja kofuli hiyo na kufanikiwa kufungua mlango  huku akidai kuwa hayuko tayari kuona waizi   wakifunga ofisi yake ambapo alisema ameshampigia katibu  wa umoja huo kuwa asiingie katika ofisi hiyo hadi baraza litakapo kaa  siku ya jumamosi kufanya maamuzi.

Awali kabla  ya tukio la kufunga ofisi kutokea  Katibu wa umoja huo Ezekiel Mollel  inasemekana  kuwa alishapewa barua ya uhamisho kutakiwa kuhama mkoa huo jambo ambalo limeleta mkinzano baina  ya uongozi wa umoja huo.

Akizungumza na Gumzo Tz  juzi ofisini  kwake Katibu huyo alipotembelewa na mwandishi wa habari hizi juu  ya jambo hilo alisema ni kweli barua ilishakuja kua  anatakiwa kuhama na tayari alishakuja mtu  kuripoti ila kamati  ya utekelezaji ilimtaka kufanya taratibu  za kutekeleza majukumu ya makabidhiano ya ofisi ili  aweze  kukabidhi  ofisi hiyo.

Hata hivyo Mollel alisema kutokana na miradi ya  umoja huo kuhujumiwa yeye amejipanga kusimamia miradi hiyo ili kuweza kuingiza  pato katika chama jambo ambalo alisema anapigwa vita.
"Haiwezekani maduka ya Chama ya biashara watu wanalipa sh. 5000 kwa mwezi hapa mjini  huku watu wachache wakifaidi mamilioni ya pesa na sisi kupata kiasi kidogo namna hii  hiyo nitaipiga vita na ninajua kuna kikundi cha watu wachache wanatafuta kuniondoa ili waendelee kula" alisema Mollel.

Alisema  lengo lake siyo kung' ang' ania ofisi  bali  anatetea maslahi ya  vijana yasiendelee kuwa mikononi mwa watu wachache.
Kufuatia mgogoro  huo  kada wa chama hicho  Amoni Filemoni   ameshikiliwa na jeshi  la polisi kwa upelelezi zaidi.

HAKUNA ATAKAEFUNGUA OFISI ASEMA MWENYEKITI UVCCM ARUSHA HAKUNA ATAKAEFUNGUA OFISI ASEMA MWENYEKITI UVCCM ARUSHA Reviewed by KUSAGANEWS on September 15, 2016 Rating: 5

No comments: