WATUMBULIWA KWA KUSABABAISHA HASARA YA SHILINGI MILIONI MBILI KATIKA KITUO CHA AFYA CHA KALOLENI ARUSHA


Mkurugenzi wa jiji la Arusha Bw Athumani  Juma Kihamia

Mkurugenzi wa Jiji la Arusha Bwana Athumani Kihamia amewasimamisha kazi watumishi wawili wa Idara ya Afya kutoka Kituo cha Afya Kaloleni ambao ni Mfamasia Zephania Ntaturu na msimamizi wa maabara Joyce Kitinye kwa kosa la upotevu wa Dawa na Vitendanishi vyenye thamani ya shilingi milioni 2.

Mkurugenzi Kihamia amefikia uamuzi huo mara baada ya kupokea malalamiko kutoka kwa watu mbalimbali na hatimaye kufanya kikao kilichojumuisha Mganga mkuu wa Jiji na Uongozi wa Kituo cha Afya Cha Kaloleni.

Katika Kikao hicho watuhumiwa walikiri kuhusika na upotevu wa dawa na vitendanishi hivyo na kuomba kurejesha fedha mwisho wa mwezi Septemba mwaka huu; zenye dhamani ya vifaa na dawa zilizopotea jambo ambalo mkurugenzi Kihamia hakukubaliana nalo;kwa kuwa suala hilo ni wizi wa mali ya umma.

Aidha Mkurugenzi wa Jiji amewataka Watumishi wote kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia kanuni, sheria na taratibu za Utumishi wa Umma; na kuonya kwamba hakuna mtumishi atakayebaki salama kwa kwenda kinyume na miiko ya utumishi wa Umma.

Pia Mkurugenzi amemwagiza Mkaguzi wa ndani kufanya ukaguzi katika vituo vya afya na zahanati zilizopo katika Halmashauri ya Jiji la Arusha; ili kujua kama kuna wizi wa dawa na vifaa ama la.
WATUMBULIWA KWA KUSABABAISHA HASARA YA SHILINGI MILIONI MBILI KATIKA KITUO CHA AFYA CHA KALOLENI ARUSHA WATUMBULIWA KWA KUSABABAISHA HASARA YA SHILINGI MILIONI MBILI KATIKA KITUO CHA AFYA CHA KALOLENI ARUSHA Reviewed by KUSAGANEWS on September 19, 2016 Rating: 5

No comments: