Nigeria kuchaguwa magavana na wabunge


 Wapiga kura nchini Nigeria watapiga kura leo kuchagua magavana wa majimbo pamoja na wabunge.
Chama cha APC kinatarajiwa kupata ushindi mkubwa baaada ya mgombea wake wa urais Muhammadu Buhari kumshinda rais Goodluck Jonathan wiki mbili zilizopita.

Hata hivyo chama cha bwana Jonathan cha PDP kinatarajiwa kupata ushindi kwenye maeneo mawili likiwemo eneo la Lagos ambalo huchangia theluthi moja ya uchumi wa Nigeria pamoja na jimbo lenye utajiri wa mafuta la Rivers.

Usalama unatarajiwa kuwa wa juu kutokana na hofu ya mashambulizi kutoka kwa kundi la Boko Haram.
Nigeria kuchaguwa magavana na wabunge Nigeria kuchaguwa magavana na wabunge Reviewed by KUSAGANEWS on April 11, 2015 Rating: 5

No comments: